Ijumaa, 28 Oktoba 2011

VIPIMO VYA UKIMWI VYA NYUMBANI VINATIA SHAKA.

Onyo juu ya vipimo vya Ukimwi

Moja ya aina ya kipimo cha nyumabani cha HIV.
Vipimo haramu vya nyumbani vya kupimia HIV vinawapa watu matokeo yasiyo sahihi, shirika la kudhibiti dawa na huduma za afya (MHRA) limeonya.
Limesema kuna matatizo mengine pia kwenye vipimo vya magonjwa ya zinaa ambayo ni halali lakini huenda pia vikawa si sahihi.
Chombo hicho kinaufanyia uchunguzi mtandao wa Uingereza unaouza vifaa hivyo.
Wakala wa kulinda afya umewaandikia baadhi ya walioathirika na kuwaeleza kuwa vipimo hivyo havikubaliki.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni