Monday, June 4, 2012

KIKWETE ATEMBEA MITAA YA ARUSHA HUKU AKIFANYA MAZOEZI, WANANCHI WAFURAHISHWA.


Rais Jakaya Mrisho Kikwete, aliye katika mapumziko mafupi jijini Arusha, akiwa katika mazoezi yake ya kutembea kilomita tatu kila asubuhi na jioni kabla ya kufanya mazoezi ya viungo na kuingia gym, katika kuuweka mwili wake katika hali ya ukakamavu na afya. Wakaazi wengi wa Arusha ambao wamemuona akitembea wamesisimkwa na kufurahishwa sana na hatua hiyo ya kiongozi mkuu wa nchi kuwa mstari wa mbele katika kujenga afya kwa mazoezi ya kila siku, na kutaka kila mtu, si viongozi tu, kuiga mfano wake.PICHA NA IKULU.
 
Mkuu wa Nchi akiwapeleka puta wasaidizi wake wakati wa mazoezi ya jioni akiw amapumzikoni huko Arusha hivi karibuni, safi sana Mkubwa nasi pia tunaanza leo.

PICHA YA LEO; MJUE FARID HADI, KIONGOZI WA KUNDI LA UAMSHO LA ZANZIBAR.


Huyu ndiye Kiongozi wa Kundi linalojiita UAMSHO la Zanzibar ambalo ni la shughuli za mihadhara ya Kidini hasa ya Kiislam lakini kwa sasa limejinasibu kupigania Zanzibar ijiondoe katika Muungano wa Tanzania katika mtindo wa vurugu za kuchoma moto sehemu za ibada za wale wasiokuwa Waislam na sehemu za biashara za Watu toka Tanganyika. Huyu jamaa na wenzie wanaelewa kweli gharama ya ubaguzi wanaouanzisha kwa kivuli kisicoeleweka kama ni siasa au dini, ingekuwa enzi ya mwalimu tungeshamdhibiti na adabu angekuwa nayo maana anajidai hata dola haogopi. Huo ni mtazamo wangu tu Wazee sijui wenzangu mnamuonaje, yupo kwenye njia sahihi ya kile anachopigania!!!!!?
 Katiba ya JMT inaruhusu uhuru wa kutoa mawazo lakini uhuru huu usiingilie uhuru wa mwingine, Tume ya Rais ya Kukusanya maoni ya Katiba mpya ndio kwanza imeanza kazi na ni nafasi nzuri tu ya UAMSHO kutoa dukuduku zao katika Tume hiyo badala ya kuharibu utulivu wa Nchi na Watu wake.

Sunday, June 3, 2012

NAPE NNAUYE ATIKISA SONGEA LEO


Chama Cha Mapinduzi (CCM) leo kimeiteka Songea baada ya umati wa wananchi wa mji huo kujitokeza katika mkutano wa hadhara wa CCM uliohutubiwa na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye  kwenye Uwanja wa Zimanimoto mjini Songea mkoani Ruvuma. Pichani, Nape akiwasalimia wananchi baada ya kuwasili kwenye uwanja huo. Kushoto ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Ruvuma Cornel Msuha. Pia alipata fursa ya kuongea na Jumuiya za wanafunzi wa Vyuo vya Elimu ya Juu vilivyopo mjini Songea. (Picha na  Bashir Nkoromo)

MBUNGE WA BAHI CCM AKAMATWA KWA RUSHWA YA MILIONI MOJA.

Mbunge wa Jimbo la Bahi (CCM), Omary Badwel
Neville Meena na Fidelis Butahe

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) inamshikilia Mbunge wa Jimbo la Bahi (CCM), Omary Badwel kwa tuhuma za kupokea rushwa ya Sh1 milioni kutoka kwa kiongozi wa Serikali.

Habari zilizopatikana na kuthibitishwa na Mkurugenzi wa Upelelezi wa taasisi hiyo, Alex Mfungo zinaeleza kuwa Badwel alikamatwa na maofisa wa Takukuru jana saa 9:00 alasiri katika Hoteli ya Peacock jijini Dar es Salaam.

Badwel ambaye ni mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) anadaiwa kukamatwa wakati anapokea rushwa kutoka kwa maafisa wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani jana.

Mfungo aliliambia Mwananchi Jumapili kuwa wanaendelea kumshikilia huku wakati wanafanya uchunguzi hadi kesho ambapo watamfikisha mahakamani.

“Siwezi kumtaja aliyekuwa akitoa rushwa kwa sababu bado tunaendelea na upelelezi, ila mpaka sasa yuko mahabusu na tutamfikisha mahakamani Jumatatu(kesho),” alisema Mfungo.

Alisema kuwa mbali na kumfikisha mahakamani, pia watatoa taarifa zaidi za tukio hilo kesho.
SOURCE; Mwananchi via Kapinga's blog.

Saturday, June 2, 2012

PICHA YA LEO; TAFAKURI YA AFYA NA UCHUMI, WEWE UNASEMAJE!!!?

RAIS WA ZAMANI WA MISRI AFUNGWA KIFUNGO CHA MAISHA JELA, WATOTO WAKE WAACHIWA HURU.

Cairo (CNN) -- Ousted Egyptian leader Hosni Mubarak was sentenced to life in prison Saturday after he was convicted of ordering troops to open fire on demonstrators, a verdict that saw angry protesters disrupt the proceedings.

Punches were thrown as victims' family members protested the verdict inside the court. Others stood on chairs, raising fists in the air and chanting the sentence was not enough.
Mubarak and the judge were removed from the courtroom amid the melee.
The sentence handed down by Judge Ahmed Refaat was the final chapter of Mubarak's three decade, iron rule of Egypt that was brought to an end in February 2011.

The last days of Hosni Mubarak's regime
Egypt one year after uprising
Could Mubarak be sentenced to death?
Before a packed courtroom, Refaat praised the revolution and said it offered people relief after living "in 30 years of dark without any hope."
About 840 people died and more than 6,000 others were wounded in the uprising, according to Amnesty International.
Refaat chose the lesser of two sentences. Mubarak could have received the death penalty.
Former Interior Minister Habib El Adly was also convicted of ordering security forces to kill protesters and sentenced to life in prison. El Adly was convicted in May of corruption and money laundering, and sentenced to 12 years in prison.
But Refaat cleared Mubarak's sons -- Gamal and Alaa -- and a handful of Mubarak's aides.
Mubarak and his sons arrived Saturday morning at the Cairo Police Academy, where the trial was held, under tight security. Police in riot gear lined up behind a barricade separating them from demonstrators.
Hundreds outside the court chanted: "Execution is the only solution" and "he who kills must die."
Families of those killed during the protests carried posters emblazoned with photos of the dead while dozens of Mubarak supporters chanted ''innocent.

Thursday, May 31, 2012

HALI YA AMANI HUKO SYRIA NI MBAYA, ANNAN AKARIBIA KUNYOOSHA MIKONO.

Koffi Annan katika Mkutano na waandishi wa Habari mjini Damascus.
Hali yazidi kuwa tete Syria
Kiongozi Mkuu wa waasi nchini Syria amemtaka Mjumbe wa Umoja wa Mataifa na Jumuiya ya nchi za Kiarabu, Koffi Annan kutangaza kuwa mpango wake umeshindwa.
Kanali Riad al Assad amesema hii itawaweka huru waasi kutokana na mpango wa kusitisha mapigano, ambao Marekani imesema unaweza kuvunjika na kusasbisha mgogoro mpana zaidi katika mashariki ya kati.
Tamko hili la kanali al Assad linakinzana na lile lililotolewa na waasi la kumpa masaa 48 rais Bashar al Assad kutekeleza mpango wa Annan. Assad aliiambia Televisheni ya Al-Jazeera kuwa hakuna muda wa mwisho lakini wanamtaka Annan atangaze kushindwa kwa mpango wake ili wawe huru kuendesha operesheni dhidi ya utawala wa rais Assad.
Majengo mjini Homs yakitoa moshi baada ya kushambuliwa. Majengo mjini Homs yakitoa moshi baada ya kushambuliwa.

Hakuna dalili za mafanikio
Mpango wa Katibu Mkuu huyo wa zamani wa Umoja wa Mataifa, haujaweza kusitisha mauaji nchini Syria na Balozi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa, Suzan Rice ameonya kuwa Baraza la Usalama lisipoushinikiza utawala wa Assad kuacha ukandamizaji wa wapinzani, mataifa yatalaazimika kuchukua hatua nje ya Umoja huo.

"Na kwa hakika hiyo ndiyo hali mbaya zaidi ambayo kwa bahati mbaya ndiyo inaelekea kutokea sasa hivi, pale vurugu zitakapongezeka na mgogoro kusambaa na kufikia kiwango cha juu cha utovu wa huruma,na kuhusisha mataifa katika kanda, na kuanza kuchukua sura ya kiitikadi na tutakuwa na mgogoro mkubwa si ndani ya Syria tu bali ndani ya kanda nzima," alisema Balozi Rice
Miili ya watu waliouawa mjini Houla ikizikwa. Miili ya watu waliouawa mjini Houla ikizikwa.

Katika hali kama hiyo, mgogoro wa Syria ambayo ina waumini wengi wa madhehebu ya sunni lakini mtawala wake wa Kabila la Alawite ana uhusiano wa karibu na dola la Kishi'a la Iran unaweza kugeuka wa uwakala ambapo silaha zitakuwa zinatoka kila kona, alisema Rice.
Mgawanyiko miongoni mwa wapinzani
Matamshi kutoka kwa waasi, yanaonyesha namna wapinzani wa rais Assad wamegawanyika, zaidi ya miezi 14 tangu kuanza kwa harakati za ukombozi wa Syria. Waangalizi wa Umoja wa Mataifa waliripoti siku ya Jumatano kuwa waligundua miili ya watu 13 waliouawa na kuzikwa pamoja Mashariki mwa Syria, siku chache baada ya mauaji ya watu 108 katika mji wa Magharibi wa Haula ambapo jeshi na wanamgambo watiifu kwa utawala walishtumiwa kwa mauaji hayo.

Balozi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa Susan Rice Balozi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa Susan Rice

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-Moon ameonya kuwa janga kubwa linaelekea kuitumbukiza Syria katika vita vya maafa makubwa ambapo kamwe madhara yake hayatakuja kuisha. Akizungumza mjini Istanbul, Ban alisema mauaji ya raia wasio na hatia, kama yaliyoshuhudiwa wiki iliyopita yanaweza hayapaswi kuendelea na kwamba jumuiya ya kimataifa inaitaka Syria kutekeleza wajibu wake kwa raia.
Wakati huo huo, Urusi na China zinaendelea kushikilia msimamo wao wa kupinga hatua zozote za kuingilia kijeshi nchini Syria na Urusi imesisitiza kuwa msimamo wake huo bado uko pale pale.
Mwandishi: Iddi Ismail Ssessanga\APE\RTRE
Mhariri: Mohammed Abdul Rahman

Tuesday, May 29, 2012

AJINYONGA KWA MADAI YA UGUMU WA MAISHA


Jamaa akiwa ananing’inia muda mchache baada ya kujinyonga.
Marehemu akionekana kwa nyuma.
Mke wa marehemu akilia kwa uchungu.
Baada ya kuteremshwa chini na Wasamaria wema.
Majirani waliokusanyika eneo la tukio.
----
MWANAMME mmoja ambaye hakutambulika jina lake, aliyekuwa mkazi wa Kigogo-Mbuyuni jijini Dar es Salaam asubuhi ya kuamkia leo (Mei 29), amejinyonga kwa madai ya ugumu wa maisha uliosababishwa na kukosa ajira.
Wakizungumza na mtandao wa huu, baadhi ya majirani ambao walihojiwa walisema kuwa jamaa huyo kwa muda mrefu alikuwa hana kazi hivyo kumsababishia ugumu wa maisha ambao ulikuja kumfanya ajinyonge.
“Siku zote mwanaume ameumbwa kutafuta riziki na si kukaa kusubiri kuletewa riziki. Jamaa huyu alikuwa akikaa tu nyumbani akimuachia mkewe aende akatafute riziki, matokeo yake ndio haya,” alisema jirani mmoja aliyekuwepo eneo la tukio.
Credits (Picha/ Habari: Shakoor Jongo /GPL)

MLIPUKO WA NAIROBI WAHUSISHWA NA UGAIDI WA KUNDI LA AL SHABAAB.



Mlipuko wajeruhi 33 Nairobi Kenya, polisi wasema huenda ni ugaidi
Polisi nchini Kenya inasema mlipuko uliojeruhi watu 33 katika mji mkuu Nairobi unaweza kuwa umesababishwa na bomu, baada ya hapo awali kulaumu hitilafu za umeme.
Mlipuko huo uliharibu maduka katika barabara yaMoi Avenuewakati wa mchana.Mtu mmoja aliyeshuhudia alisema kifurushi kiliachwa karibu yake kabla ya mlipuko kutokea.
Waziri Mkuu Raila Odinga amesema mlipuko huo unahusiana na magaidi.
Mwandishi wa BBC Kevin Mwachiro anasema mlipuko huo umesababisha bidhaa mbali mbali kama viatu, nguo na vioo vilivyovunjika kusambaa sehemu yote ya eneohilo.
Picha za Televisheni nchini humo zilionyesha watu wakikimbia mbali na majengo yaliyo karibu katikati ya mji waNairobi.
Awali Kamishna wa Polisi nchini Kenya Mathew Iteere, alisema huenda "hitilafu ya umeme" ndio chanzo cha mlipuko huo, kwa mujibu wa Televisheni ya NTV. Hata hivyo mlipuko huo unaiwekaNairobikatika hali ya wasiwasi.
Kumekuwa na milipuko kadhaa hivi karibuni ndani na nje ya mji huo mkuu huku baadhi ikihusishwa na kundi la wapiganaji wa Al-Shabaab.
Polisi waliweka kizuizi eneo la mlipuko huo Nairobi.
Timu ya waokoaji wa Shirika la Msalaba Mwekundu imetumwa katika eneo la tukio kwenye barabara ya Moi. Mtaa huo ni barabara kuu ambayo wakati wa mchana huwa na watu wengi, Shirika la habari la AP linasema.
Kwa mujibu wa watu walioshuhudia kulikuwa na mlipuko mkubwa na huku vipande vipande vya vioo na vitu vingine vikiwarukia na kujeruhi watu waliokuwa karibu, Gazeti la Nation linaripoti

WANA UAMSHO ZANZIBAR WAMEPEWA DHAMANA JANA.

Watu thelathini waachiliwa kwa dhamana kufuatia ghasia mjini Zanzibar
Viongozi wawili wa kundi la Uamsho waliokuwa wanashikiliwa na polisi wa Zanzibar kwa zaidi ya siku mbili pamoja na baadhi ya wafuasi wao wameachiwa kwa dhamana katika mahakama ya Mwanakwerekwe huko mjini Zanzibar.
Kwa mujibu wa wachambuzi wa mambo ya kisiasa, kuachiwa kwa viongozi hao ambao walikuwa wanakabiliwa na kosa la kuandamana bila kibali kunaweza kukomesha uhasama wa takriban siku mbili baina ya wafuasi wa kundi hilo na polisi.
Mwandishi wetu Aboubakar Famau aliyekuwa Zanzibar anasema hali ilianza kuwa shwari mjini Zanzibar baada ya kuachiliwa kwa dhamana kwa wafuasi takriban thalathini wa kundi la Uamsho waliokuwa wanashikiliwa na polisi mjini humo kwa tuhuma za kuandamana bila kibali.
Miongoni mwa waliopata dhamana hiyo ni Sheikh Mbaruku Saidi Khalfan na Musa Juma Musa wote wakiwa viongozi wa kundi hilo ambao kukamatwa kwao kumeleta kizazaa mjini humo.
Mbele ya Hakimu wa mahakama ya Mwanakwerekwe majira ya saa nne asubuhi Jumatatu, baada ya kusomewa mashtaka ya kufanya mkusanyika haramu katika maeneo mbalimbali ya Zanzibar, watuhumiwa hao kwa pamoja walikana tuhuma hizo.
Baadaye wakili wa watuhumiwa hao aliwaombea dhamana, ombi ambalo lilikubaliwa bila pingamizi lolote.
Kukamatwa kwa viongozi hawa kumeleta sokomoto kubwa mjini Unguja hasa baada ya wafuasi wa kundihilokuamua kuandamana kwa lengo la kuishinikiza polisi kuwaachia.
Hali iliyosababisha vuta nikuvute baina ya wafuasi hao na polisi ambao wamekuwa wakitumia mabomu ya kutoa machozi na maji ya kuwasha.
Uamsho ni kundi la kidini ambalo limejipa jukumu la kuwaelimisha wazanzibari kuhusu suala la muungano hasa wanapotoa maoniyaokatika Tume ambayo inakusanya maoni ya wananchi kuhusu katiba mpya. Hata hivyo, taarifa zisizothibitishwa zinasema, kundihilolimejikita zaidi katika kuwahamasisha wananchi kuupinga muungano

Sunday, May 27, 2012

ZANZIBAR HALI SI SHWARI TENA, KANISA LA ASSEMBLIES OF GOD LACHOMWA MOTO, SERIKALI YAZUIA MIKUSANYIKO YOYOTE.

Kumbe Zanzibar tatizo si muungano bali udini?



Baada ya polisi wa kupambana na ghasia kutunishiana mikono na kundi la JUMIKI au Jumuia ya Uamsho na  Mihadhara ya Kiislamu kanisa la Tanzania Assembly of God (TAG) la mtaa wa Kariakoo Zanzibar limechomwa usiku wa kuamkia leo. Je hii ni bahati mbaya au kuna ushirika wa kundi hili linaloanza kutishia amani ya nchi? Tunaambiwa watu wasiojulikana wamechoma kanisa hili. Je kweli waliochoma hawajulikani wakati dalili zote zinaelekea kwa JUMIKI? Kuna haja ya serikali kuwa serious na kundi hili ambalo lina kila alama za kigaidi. Hata Al Shabaab ilianza hivi. Maana bado kuna wendawazimu wanaodhani nchi inaweza kutawaliwa kidini. Hii si karne ya saba na kumi na nne.Je tatizo la Zanzibar ni muungano au udini

STANSLAUS BONIFACE AFARIKI DUNIA, NI YULE MWENDESHA MASHTAKA KESI ZA EPA, R I P BROTHER.

MKURUGENZI Msaidizi wa Mashitaka nchini na Mwendesha Mashitaka mashuhuri katika kesi kubwa mbalimbali nchini, Stanslaus Boniface amefariki ghafla.

Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana jana mchana na kuthibitishwa na Mkurugenzi wa
Mashitaka (DPP), Eliezer Feleshi, Boniface alifariki ghafla jana asubuhi na chanzo cha kifo chake hakijafahamika.

“Boniface amefariki leo (jana) alfajiri katika Hospitali ya Regency alikopelekwa baada ya kujisikia vibaya akiwa nyumbani kwake…msiba upo nyumbani kwake eneo la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam,” alisema Ofisa Habari wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu (AG), Siatu Msuya.

Boniface alipata umaarufu katika kesi alizokuwa akiziendesha ambazo ni za wizi wa fedha za Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) katika Benki Kuu (BoT) ikiwamo inayomkabili kada wa CCM, Rajab Shaban Maranda na wafanyakazi wanne wa BoT wanaodaiwa kuiba Sh 207,284,390.44.
.


Mkurugenzi wa Mashtaka Nchini, Ndg. Eliezer Feleshi

Nyingine ni ile ya wizi wa Sh bilioni 1.1 inayomkabili Bahati Mahenge na wenzake wanne.

Boniface alizaliwa Februari 21, 1968 na ameacha mke na watoto watatu. Amewahi kufanya kazi kama Mwendesha Mashitaka Mkuu katika mikoa ya Mwanza, Mbeya na Dar es Salaam

WAVULANA WATATU WAFANYIWA UPASUAJI KUONDOA MATITI YALIYOTOKANA NA UWINGI WA HOMONI ZA UKUAJI MAZIWA. KITAALAMU HALI HII HUITWA 'GYNECOMASTIA', WANASEMA WALIKUWA WANACHEKWA NA WENZAO. NI HUKO JAMHURI YA DOMINICA.

A trio of brothers who grew breasts due to a rare genetic disorder are now 'living a normal life' after going under the knife.
The Ramírez brothers, from the Dominican Republic, said they were 'extremely happy' they were no longer being bullied, beaten and ridiculed for their 'moobs'.
Yeuri, 17, told local TV: 'It hurt a lot but now I feel good. Now they can't make fun of us anymore.'
Dominican Republic boys Dominican Republic boys
Surgery: A trio of brothers went under the knife because they developed breasts due to a genetic condition
Rare: The trio of brothers who grew breasts due to a rare genetic disorder are now 'living a normal life' after going under the knife
Rare: The trio of brothers who grew breasts due to a rare genetic disorder are now 'living a normal life' after going under the knife

The plight of the siblings, which some have described as a hoax, was highlighted when their desperate father Felipe appealed for help, via the island's news programme Zona5, from specialists.
His work as a food stall seller, and the absence of the boys' mother who left when they were little, meant he did not have enough money to pay for an operation.

His emotional plea was picked up by medics at the Marcelino Velez Santana Hospital, whose boss Dr Pedro Antonio Delgado agreed to pay for the operations.
After tests to see if Yeuri, his 11-year-old brother Gabriel and 12-year-old Daniu could undergo treatment, they each went under the knife for two hours.
Ecstatic: Felipe Ramirez, pictured here with one of his sons in the background, said he was thrilled with the outcome of the surgery
Ecstatic: Felipe Ramirez, pictured here with one of his sons in the background, said he was thrilled with the outcome of the surgery
Dr Pedro Antonio Delgado Dr Elbi Morla told the show: 'In reality, this is a key moment in their evolution. It was something that was affecting them greatly.'
Medics: Dr Elbi Morla (up) said the operation would be a key moment in the boy's lives, while Dr Pedro Antonio Delgado (down) confirmed his hospital paid entirely for the surgery

Rare: The condition affected the boys who are from the southern rural town of Magueyal
Rare: The condition affected the boys who are from the southern rural town of Magueyal
After the operation, for the condition called gynecomastia which affects males who have a hormonal imbalance, Dr Elbi Morla told the show: 'In reality, this is a key moment in their evolution.
'It was something that was affecting them greatly.'
And a grateful Felipe added: 'They are now normal men. They have had them taken off. I never had the hope that this would happen.
'I never had the money to do this. I'm so thankful to the press for helping.'
Happy familiy: Felipe Ramirez (right) with his three sons after their operation and a presenter from Zona5, which was instrumental in organising their surgery
Happy familiy: Felipe Ramirez (right) with his three sons after their operation and a presenter from Zona5, which was instrumental in organising their surgery

 Doctors said they will now monitor the boys and give them medicine to block the female hormones they were producing.
And they revealed that the condition, affecting the boys from the southern rural town of Magueyal, was genetic.
It was most likely due to a hormonal anomaly passed on through generations of the area’s small congenital gene pool.

Friday, May 25, 2012

MNYIKA ASHINDA KESI YA UCHAGUZI, NI MBUNGE HALALI WA UBUNGO.


Mh. John Mnyika alipokuwa anawasili Mahakama Kuu jana asubuhi.

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), jana kilikuwa katika furaha baada ya Mbunge wake wa Ubungo, John Mnyika kuthibitishwa na Mahakama Kuu kuwa Mbunge halali wa Ubungo jijini Dar es Salaam.

Ubunge wa Mnyika ulikuwa unapingwa katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam na aliyekuwa mgombea wa CCM, Hawa Ng’humbi.

Mahakama hiyo jana kupitia kwa Jaji Upendo Msuya, ilitamka kuwa uchaguzi katika jimbo hilo ulikuwa wa halali na kura alizopata Mnyika ni halali.

Aidha, Jaji Msuya alisema maombi ya Ng’humbi kuwa mahakama hiyo ibatilishe matokeo yaliyompa ushindi Mnyika yametupwa kwa kuwa hakuthibitisha madai yake na kutakiwa kulipa gharama za kesi hiyo aliyoifungua mwaka 2010, siku chache baada ya kubwagwa na kijana huyo.

Awali kabla ya kusomwa kwa hukumu hiyo, Mahakama hiyo jana ilijaa wanachama na wapenzi wa Chadema na CCM na kusababisha askari Polisi kufanya kazi ya ziada ya kutanda kila mahali katika mahakama hiyo na katika Barabara ya Kivukoni kuanzia Mahakama ya Rufaa wakiwa na magari ili kuimarisha ulinzi.

Hukumu hiyo ilisomwa na Jaji Msuya mahakamani hapo kwa takribani saa moja na nusu kuanzia saa 4 asubuhi ambapo pia amuru gharama za kesi hiyo kubebwa na Ng’humbi ambaye kabla ya kuwania ubunge mwaka 2010, alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma.

Jaji Msuya alisema Ng’humbi katika madai yake yote matano hakuna hata moja alilolithibitisha kama ambavyo sheria inamtaka mdai katika kesi ya uchaguzi, kuthibitisha dai lake bila kuacha shaka yoyote na kutoa ushahidi kuonesha ni namna gani iliathiri matokeo ya uchaguzi.

Alisema Ng’humbi na mashahidi wake aliowaita mahakamani, hawakuonesha wala kuthibitisha madai yaliyowasilishwa hapo kwamba yalitendeka na namna gani madai hayo yaliathiri matokeo ya uchaguzi uliofanyika Oktoba 31, mwaka juzi.

“Nilipata nafasi ya kupitia ushahidi wa kila shahidi pamoja na vielelezo vilivyotolewa mahakamani katika kesi hii, lakini nimeshangaa ni kwa nini mdai hakuleta mahakamani mashahidi ambao walikuwepo katika chumba cha majumuisho ya kura ambako ndiko madai hayo yalikotokea,” alisema Jaji Msuya.

Alisema hakuelewa ni kwa nini watu zaidi hawakuletwa kuunganisha ushahidi wao kuthibitisha madai ya mdai na kuhoji kama kweli madai hayo yalitokea, ni kwa nini wagombea wengine au watu waliokuwa katika chumba cha majumuisho hawakulalamika?

Katika madai ya Ng’humbi ya dosari ya kura zaidi ya 14,000 alizodai hazieleweki zimetoka wapi, Jaji alisema alipata nafasi ya kuhesabu kura walizopata wagombea wote wa vyama vilivyogombea jimbo hilo ambavyo ni 16 na kubaini ilikuwa ni kosa tu la kibinadamu na halina uhusiano wowote na mdaiwa wa pili, Mnyika.

Kwa mujibu wa Jaji Msuya, fomu namba 24 b ilikuwa na dosari na ndiyo ilikuwa inabishaniwa na Ng’humbi kwa kuwa ilikosewa kuandika.

Alisema Mnyika alitangazwa kuwa ni mshindi baada ya kupata kura 66,742 wakati Ng’humbi alipata kura 50,544 na wagombea wote kuwa kura 132,496.

Jaji Msuya alisema katika ushahidi wa Ng’humbi, hakuonesha ni vipi ongezeko hilo la kura liliathiri matokeo ya uchaguzi na vipi Mnyika alihusika na ongezeko hilo.

Kabla ya kuanza kuchambua hoja za Ng’humbi, Jaji Msuya aliwapongeza mawakili katika kesi hiyo ambao walijitahidi kuwasilisha mashahidi na kuhoji maswali ya msingi.

Alisema mawakili hao hawakupoteza muda kwa kuuliza maswali yasiyo na msingi wala kuwasilisha pingamizi zinazosababisha shauri kuwa na mlolongo mrefu.

Mnyika aliwakilisha na wakili Edson Mbogoro wakati wakili wa Ng’humbi alikuwa Issa Maige na Mwanasheria Mkuu wa Serikali aliwakilishwa na Justus Mlokozi.

Kuhusu madai ya Ng’humbi kuwa alidhalilishwa kwa kuitwa fisadi na Mnyika katika mkutano alioufanya katika kampeni kwamba aliuza nyumba ya Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi Tanzania (UWT), na kwamba watu wasichague CCM inakumbatia mafisadi, Jaji Msuya alisema hayakuwa na ushahidi.

Alifafanua kwamba Ng’humbi alidai maneno hayo yalizungumzwa na Mnyika katika mkutano uliokuwa na watu zaidi ya 500, lakini yeye hakuwapo. Kutokana na kukosekana kwa uwepo wake, Jaji Msuya alisema Mahakama haichukui maneno ya kuambiwa, bali mtu aliyesikia mwenyewe au kushuhudia.

“Katika watu wote hao 500 waliokuwa katika mkutano huo, hakuja hata mtu mmoja kutoa ushahidi na pia haikuthibitishwa ni namna gani iliathiri uchaguzi na hivyo hoja hiyo imeondolewa,” alisema Jaji Msuya.

Kuhusu madai kwamba Mnyika aliingia na wafuasi wengine wa Chadema katika kujumlisha matokeo, Jaji Msuya alisema ushahidi pekee ni wa Ng’humbi na kwamba hadhani kuwa ni jambo linalowezekana mtu asiyehusika kuingia katika chumba cha majumuisho ya kura wakati kulikuwa na ulinzi.

Alisema mbali na ulinzi, hata wagombea wengine wangelalamikia jambo hilo, lakini Ng’humbi hakuleta mashahidi waliokuwa katika chumba hicho kutoa ushahidi kuwa kuna watu wasiohusika waliingia.

Kuhusu madai kuwa Msimamizi wa Uchaguzi alitumia kompyuta za mkononi (laptop) za Mnyika badala ya kompyuta rasmi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na pia hazikukaguliwa kiasi cha kutia shaka kuwa pengine kulikuwa na taarifa zisizo rasmi katika kompyuta hizo ikiwa ni pamoja na ongezeko lile la kura 14,000, Jaji Msuya alisema ushahidi umeonesha kuwa kompyuta hizo hazikutumika.

Alifafanua kwamba kompyuta zilizotumika zilikuwa za mawakala na kwamba katika madai hayo, Ng’humbi angeweza kuleta mashahidi zaidi kuthibitisha akiwemo aliyekuwa Mkurugenzi wa Uchaguzi, Rajab Kiravu.

“Tofauti ya kura kama nilivyosema nimepiga hesabu na nimeona kuwa ni matatizo ya kibinadam na hakuna athari yoyote katika matokeo ya uchaguzi, ni shahidi wa tatu pekee aliyekuja kutolea ushahidi hili na Ng’humbi angeweza kuleta mashahidi zaidi,” alisema Jaji Msuya ambaye alianza kuisikiliza kesi hiyo kuanzia Aprili 19, mwaka huu na majumuisho ya pande zote yalifanywa Mei 4, mwaka huu.

Baada ya hukumu hiyo, Mnyika alikumbatiana na Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema, Freeman Mbowe ambaye alikuwapo mahakamani hapo. Pamoja walitoka nje, Mnyika akiwa amebebwa na wafuasi wa Chadema wakiimba na kushangilia kwa ushindi huo.

Hata hivyo, hakukuwa na vurugu kubwa zilizokuwa na madhara zaidi ya maandamano yaliyoondoka mahakamani hapo wakiimba.

Mbowe aliwaeleza waandishi wa habari kuwa kesi hiyo imetumia zaidi ya Sh bilioni mmoja na kutaka kabla ya kusikiliza kesi kama hiyo, uchunguzi ufanyike kwanza ili ikionekana haina hoja za msingi, itupwe mapema.

“Mahakama imetenda haki na hii inaonesha namna ambavyo inaweza kutenda haki hata katika vyama vya upinzani,” alisema Mbowe.

Naye Ng’humbi alisema amepokea uamuzi uliotolewa, lakini hawezi kusema lolote kwa sasa na kuwataka wana CCM wawe na utulivu kwa sababu anaamini ni watulivu na kama kuna jambo tofauti, atazungumza baadaye.

Hadi sasa, Mahakama imekwisha kutengua matokeo ya ubunge ya mwaka 2010 katika majimbo mawili pekee, Arusha Mjini kwa Godbless Lema wa Chadema na Sumbawanga Mjini lililokuwa la Aeshi Hilary wa CCM.

Majimbo ambayo kesi zao zilitupwa na mahakama na wabunge wake kuendelea na nafasi zao ni Segerea, Kasulu Mjini, Biharamulo, Singida Mashariki, Ilemela, Nyamagana, Kilwa Kusini, Muhambwe na Meatu

PICHA YA LEO; MSAFIRI KAFIRI.


Punda afe mzigo ufike, unaikumbuka methali hii? Bahati yao ni kwamba gari ni zuri tu na barabara pia ni nzuri, sasa tatizo sijui ni nini? Anataka kuharibu gari lake maana kalichoka ili anunue jingine!!! sijui, au anabana mafuta kwa kuogopa kurudiarudia safari, mzigo ukifika faida njenje kwa mwenye mzigo ila ni hasara ya service ya gari kwa mwenye chombo. Tutafakari  kwa pamoja je haya ni matumizi sahihi ya nyenzo zetu tulizonazo zinazotusaidia kazi mbalimbali!!?

LLOYD NCHUNGA AJIUZULU UONGOZI WA YANGA JANA.

MWENYEKITI wa Yanga, Lloyd Nchunga ametangaza kujiuzulu wadhifa huo kuanzia jana.

Kujiuzulu kwa Nchunga itakuwa furaha kwa Baraza la Wazee la Yanga, ambalo karibu mwezi mzima sasa limekuwa likimshikia bango Nchunga aachie madaraka kwa madai ya timu hiyo kufanya vibaya katika Ligi Kuu Tanzania Bara iliyomalizika mapema mwezi huu, ambapo Yanga ilishika nafasi ya tatu.
Image

Lloyd Nchunga.

Pia itakuwa imewarahisishia kazi baadhi ya wanachama wa Yanga, ambao walikutana makao makuu ya klabu hiyo makutano ya mitaa ya Twiga na Jangwani na kutangaza kumpindua Nchunga, uamuzi ambao ulipingwa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kwamba ni kinyume cha Katiba.

Uamuzi huo wa Nchunga kujiuzulu aliutangaza jana kwenye mkutano wake na waandishi wa habari uliofanyika ofisini kwake jengo la NSSF, Dar es Salaam na kwamba amefanya hivyo kwa maslahi ya Yanga.

Alisema uamuzi wake wa kujiuzulu umekuja wakati walishakubaliana kwenye kikao cha
Kamati ya Utendaji ya Yanga kwamba wajumbe wengine waliobaki wasijiuzulu hadi mkutano mkuu wa wanachama Julai 15 mwaka huu, lakini mazingira yamemfanya afikie uamuzi huo na kwamba anajua wenzake watasononeka sana.

“Nawashukuru wajumbe kwamba tulifanya kazi kwa pamoja na kwa ushirikiano mzuri, na hata pale tulipotofautiana tulifanya hivyo kwa hoja na kufikia maazimio ambayo wote tulikuwa tunawajibika nayo,” alisema.

Nchunga aliorodhesha mafanikio mbalimbali ambayo uongozi wake uliyapata tangu aingie madarakani Julai 2010, ambayo ni Ngao ya Hisani mwaka 2010, ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara mwaka 2010/2011 na ubingwa wa Kombe la Kagame mwaka 2011.

Pia alisema chini ya uongozi wake waliua uteja kwa Simba, ukiacha matokeo mabaya ya kufungwa mabao 5-0 waliyoyapata kutoka kwa Simba Mei 6, mwaka huu.

“Hata hivyo doa limetupata baada ya kufungwa na watani wetu mabao 5-0, ambapo kuna wanachama wanaoelewa na wasioelewa kabisa.

Ninachokiona mimi ni usaliti wa hali ya juu uliombatana na matukio mbalimbali yaliyopita na yanayoendelea hadi kujaribu kupindua uongozi wa halali wa kidemokrasia.

“Siwatuhumu wachezaji moja kwa moja, isipokuwa mfululizo wa matukio wiki tatu kabla ya mchezo ule na sasa, inaonesha kwamba kulikuwa na usaliti mkubwa ambao sisi hatukuweza kuubaini mapema. “Sioni mantiki katika hoja kwamba wachezaji walikuwa wakidai mishahara, posho n.k. Au ati mtendaji wetu alishikiliwa Arusha kwa deni la hoteli, ndiyo tuvune bao 5!

“Kwa wanaoijua Yanga, imewahi kuwa na madeni makubwa katika hoteli mbalimbali, mawakala wa ndege n.k, na baadhi tumeyakuta na sisi tumekuja tukayalipa. Hii imewahi kutokea kabla na wakati akiwepo mfadhili, sembuse sisi tulioachwa baki, na bado wachezaji walicheza kwa morali.

“Hata hivyo, utamaduni wa kutimuana baada ya matokeo mabaya ni dhambi ambayo itatula
kama hatutaiacha, kwani wenye hila na uchu wa madaraka wataendelea kutumia mbinu hiyo ili kuuondoa uongozi wa kidemokrasia,” alisema Nchunga.

Alieleza kuwa Jumapili baadhi ya wanachama wa Yanga walikutana na kutangaza mapinduzi, ambayo hata hivyo Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), liliyakataa.

Hata hivyo alisema baadhi ya wazee walikaririwa na kituo kimoja cha redio wakisema Yanga bora ishushwe daraja au kufungiwa kuliko Nchunga kuendelea kuongoza.

“Hii imenikumbusha hekima za Mfalme Suleiman akiamulia ugomvi wa wanawake wawili waliokuwa wakigombea mtoto naye akaamuru wagawane nusu kwa nusu. Yule mwenye mtoto kweli alimuomba Mfalme amuachie mwenzie kuliko kumkata nusu.

“Kwa hekma hiyo nimeamua kujiuzulu nafasi yangu katika uenyekiti wa Yanga kwani ni klabu
ninayoipenda hata kama sio kiongozi kwa mujibu wa ibara ya 28 ya Katiba yetu.

“Vile vile siko tayari kuona klabu yangu ikisalitiwa au kuhujumiwa eti kwa sababu tu mimi ni kiongozi. Natumaini Kamati ya Utendaji kwa pamoja na wale tuliowateua chini ya ibara ya 29(3) ya Katiba ya Yanga pamoja na Bodi ya Wadhamini, itawaongoza wanachama mpaka
kufikia mkutano mkuu kwa mafanikio zaidi.

“Nitaendelea kuwa mwanachama mwadilifu na nitatoa mchango wangu wa hali na mali pale nitakapohitajika na nikiwa na uwezo wa kufanya hivyo,” alisema Nchunga.

Nakala ya taarifa ya kujiuzulu ameituma kwa wadhamini wa Yanga, Mama Fatma Karume,
Francis Kifukwe na Yusuf Manji kwa taarifa.

Nchunga ambaye kitaaluma ni mwanasheria, alishinda uenyekiti wa Yanga Julai mwaka 2010.

Katika uchaguzi huo nafasi ya Makamu Mwenyekiti ilienda kwa Davis Mosha. Walioshinda katika ujumbe wa Kamati ya Utendaji ni Ally Mayai, Mzee Yusufu, Sara Ramadhani, Tito
Osoro, Mohamed Bhinda, Charles Mgondo, Salum Rupia na Theonest Rutashoborwa.

Hata hivyo Mosha alijiuzulu mwaka jana, wakati Mayai, Mzee Yusuph, Bhinda walijiuzulu hivi
karibuni kulipoanza shinikizo la kuung’oa madarakani uongozi wa Nchunga.

Rutashoborwa alifariki dunia