Ijumaa, 7 Oktoba 2011

MAADHIMISHO YA MIAKA 50 YA UHURU HUKO BUTIHAMA MUSOMA.


WAZIRI wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk Emmanuel Nchimbi (wa kwanza kushoto) akipata maelezo kutoka kwa maofisa wa Kampuni ya Tanzania Standard Newspapers (TSN) katika banda la kampuni hiyo kijijini Butiama mkoani Mara, kwenye maonesho ambayo ni sehemu ya maadhimisho ya wizara ya miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania Bara. Pembeni mwa Waziri ni Meneja Uchapishaji, John Mcharo aliyemwakilisha Mhariri Mtendaji katika maadhimisho; wanaotoa maelezo ni ofisa Usambazaji wa TSN, Judith Ngomo (wa kwanza kulia) na Ofisa Masoko na Mauzo, John Koyi (Picha na Stella Nyemenohi).


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni