Alhamisi, 13 Oktoba 2011

NYUMBA YA JAMBAZI SUGU YACHOMWA MOTO.

NewsImages/6001866.jpg
Nyumba ikitekea kwa moto.

Ile nyumba ya jambazi maarufu katika mkoa wa Iringa yateketezwa kwa moto na wanachi wa eneo hilo la kigamboni. Jambazi hilo kwa jina Msafiri Ilomo alikuwa akitumia nyumba hiyo kama ghala la kuhifadhia vitu vya wizi.
Ile nyumba ya jambazi maarufu katika mkoa wa Iringa yateketezwa kwa moto na wanachi wa eneo hilo la kigamboni.

Jambazi hilo kwa jina Msafiri Ilomo alikuwa akitumia nyumba hiyo kama ghala la kuhifadhia vitu aina mbalimbali ambavyo alikuwa akivinyang'anya kwa njia nguvu na vitisho ukiwa mbishi hutumia nondo kwa kumchapa binadamu mwenzie mbavuni au kichwani.

Baada ya nyumba hiyo kuteketezwa na moto jopo la wananchi walionekana wakibeba vitu vya aina malimbali kwa njia isiyo halali katika eneo hilo na kutokomea kusikojulikana.

Mheshimiwa Amani Mwamwindi ambaye ndiye meya wa Manispaa ya Iringa alifika katika eneo hilo na kushuhudia vitu vya aina mbalimbali vlivyoporwa kutoka kwa wananchi.

Mstahiki meya alisema kabla ya kukubaliana na wananchi juu ya uvunjaji wa chumba hiyo alilitaka jeshi la Polisi kuchukua mali zote kutoka kwenye nyumba hiyo,ambapo polisi wa usalama walikuwepo hapo kwa muda huo.

Tayari watu zaidi ya wawili wamepoteza maisha kwa kupigwa na jambazi hilo kwa kutumia nondo, katika hali ya kusikitisha zaidi jambazi hilo lilikuwa likiwabaka Wanawake mbalimbali.

Mheshimiwa Mwamwindi alisema kuwa amepokea kwa masikitiko makubwa juu ya tukio hilo la ujambazi katika kata hiyo ya Mwangata ambao wananchi wengi walikuwa wakiishi kwa hofu kubwa kwa kipindi kirefu zaidi.

Meya aliendelea kusema kijana Damas Kisinga amepoteza maisha kwa kupingwa na Nondo na kundi hilo la kijambazi ,kijana huyo Damas alizikwa juzi katika eneo la Makanyagio.

Majambazi hayo yalishindwa kabisa mbinu zao baada ya kuzungukwa na wananchi wakati walipovamia nyumba ya diwani wa Kata ya Mkwawa Thobias Kikula.

Mpaka sasa majeruhi waliopigwa na nondo na kukatwa na mapanga ni Michael Chengula 37 aliyevujwa mkono kabla ya kuchukuliwa simu na fedha taslimu laki moja na Mpiga picha Adilian Lusasi 45 aliyeporwa kamera yake pamoja na picha za wateja wake.

Diwani Lugenge alisema jambazi huyo alikuwa amefunga dishi la DSTV kitu ambacho wananchi wameona si cha kawaida katika nyumba hiyo ya udongo na kuitilia mashaka na kuivamia.

Bwana Lugenge aliendelea kusema takribani mwezi mmoja sasa tangu jambazi hilo lifiwe na mtoto wake ambaye aliweza kumzika kwa siri na msiba aliupeleka wa wazazi wake kwa kuhofia wananchi kujua siri kubwa ndani ya nyumba yake.

Mpaka sasa vitu vilivyokwisha kamatwa ni Nguo,Visu,DVD,TV,Sofa,Magodoro,Baiskeli,Mabati na simu aina mbalimbali, Vitanda, Vyombo vya makanisani na misikitini na mali nyingine nyingi ambazo zilijaa ndani ya chumba hiyo.

Kwa sasa vitu hivyo vipo mikononi mwa jeshi la polisi Iringa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni