Jumatatu, 10 Oktoba 2011

DK. MWAKYEMBE AUGUA UGONJWA MBAYA WA NGOZI, APELEKWA INDIA KWENYE MATIBABU, TUNAMWOMBEA KWA MUNGU APONE UPESI MPIGANAJI WETU.

Rais Kikwete alipomjulia hali Dk. Mwakyembe nyumbani kwake Kunduchi-Mtongani, Dar es Salaam hivi karibuni.

Dk. Harrison Mwakyembe akiwa na Mh Victor Mwambalaswa Bungeni Dodoma siku zilizopita
Naibu  Waziri wa Ujenzi, Dk Harrison Mwakyembe leo amepelekwa nchini India kwa matibabu zaidi ya ugonjwa wa ajabu  uliomuanza  kiasi cha miezi mitatu iliyopita kabla ya hali kubadilika siku za karibuni na hatimaye mwili wake kunza  kuvimba na ngozi kuharibika.

Msemaji wa familia ambaye pia ni Mbunge wa Lupa Mh. Victor Mwambalaswa amesema kwamba hali ya  ngozi Dk Mwakyembe ni mbaya, japokuwa ana nguvu zake na fahamu na anaongea bila shida na anatembea mwenyewe


source: http://www.wavuti.com/

Maoni 1 :