Jumapili, 9 Oktoba 2011

AJALI MBAYA YA BASI KUPINDUKA YATOKEA LEO MCHANA HUKO KILWA, NG'ITU EXPRESS YAPINDUKA NA KUACHA MAJERUHI KIBAO.

Wananchi na abiria waliokuwa wakisafiri na magari mengine njia ya kusini leo hii wakisaidia kuinua gari lililopinduka ili kuwatoa abiria watatu walionasa humo. Ajali ilitokea baada ya dereva wa basi hilo kujaribu kuyapita magari mengine bila mafanikio eneo la kati ya kijiji cha Sinza na Ngong'otela huko Kilwa.
Baada ya saa moja na nusu zoezi lilikamilika na kuwanasua abiria hao walionasa wakiwa katika majeraha mabaya baada ya kubanwa na viti vya basi hilo, majeruhi walikimbizwa katika hospitali ya Wilaya ya KINYONGA huko Kilwa.
Baadhi ya waokoaji wakijaribu kuangalia kama kuna mtu yoyote aliyebakia ndani ya basi hilo.
Manusura mmoja wa ajali hiyo aliyetambulika kwa jina la Mansour akitokea Dar es salaam kwenda Mtwara akifanya mawasiliano ya simu kuwajulisha ndugu zake kuwa kapata ajali, wengi wa abiria wa basi hilo walikuwa ni wanafunzi wa shule ya sekondari ya wasichana ya Mtwara(Mtwara Girls High School) ambao walikuwa wakielekea shuleni. Mkuu wa mkoa wa Lindi na Dar es salaam pia na Mkuu wa Wilaya ya Kilwa walikuwepo kusaidia uokoaji. Tunawaombea majeruhi wapone haraka.




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni