Ijumaa, 6 Mei 2011

WAHAMA WAKIHOFIA ULIPUAJI WA MABOMU KAMBI YA JESHI GONGOLAMBOTO.

Thursday, May 05, 2011 12:29 PM
BAADHI ya wakazi wa Gongo la Mboto walilazimika kuhama kwa kuogopa zoezi la ulipuaji wa mabaki ya mabomu katika kambi ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Gongolamboto na kurejea makazi yao jeshi hilo lilipotangaza kusitisha zoezi hilo.



Nyumba iliyoharibiwa na mabomu
Moto unaishia

Makamanda wakiangalia mabaki ya mabomu.
Wakazi hao waliondoka kwenye makazi hayo kwa hofu ya kulipukiwa na mabomu hayo kama awali japo jeshi hilo limetangaza kuwa hakutakuwa na athari yoyote kwa wakazi hao.

Jumatatu ya wiki hii jeshi hilo lilitangaza kumalizia kulipua masalia ya mabomu katika kambi hiyo na zoezi hilo kuahirishwa jana na kutangazwa.

Taarifa kutoka kwa Mkurugenzi wa Habari wa JWTZ zilidai kuwa walipanga kulipua mabomu hayo ndani ya kambi hiyo kwa kuhofia kuyalipua kwa kuyabeba kuyahamishia mahali pengine kwani kwa  kufanya hivyo kungeweza kuleta madhara makubwa.

Februari 16, mwaka huu, katika ghala la kambi ya Gongolamboto mabomu yalilipuka na kusababisha vifo vya watu 30 na wengine zaidi ya 300 kujeruhiwa huku wakazi wengine kukosa makazi na wengine kuharibiwa mali zao na mifugo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni