Jumamosi, 14 Mei 2011

WAHALIFU WAVUTIWA NA MITANDAO YA KIJAMII

Hatari zaidi katika mtandao


Utafiti uliofanywa kwa mapana kuhusiana na matumizi salama ya mtandao unathibitisha kwamba visa vya ulaghai na uhalifu vimezidi katika mitandao ya kijamii, kama vile Facebook.
Facebook
Wahalifu wanavutiwa na mitandao ya kijamii
Utafiti uliofanywa na kampuni kubwa ya Microsoft, unaonyehsa uhalifu huo umeongezeka mara 12, ikiwa ni pamoja na hali inayojulikana kama mashambulio ya 'phishing', wakati ambapo wahalifu hutumia ujumbe unaoelekea kuwa ni halali, ili kuweza kuwahimiza watumiaji mtandao kutoa maelezo yao ya kibinafsi ambayo kwa kawaida huwa ni ya siri.
Waandishi wa BBC wanaelezea kwamba kutokana na umaarufu wa mitandao ya kijamii, sio ajabu kwamba sasa wahalifu wameanza kuangazia upande huo katika kuwalenga watumizi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni