Jumapili, 8 Mei 2011

MAJESHI YA GADAFFI YASHAMBULIA BANDARI YA MISRATA.

Mabomu mtawanyiko yanatumiwa Misrata


Majeshi ya Kanali Gaddafi wa Libya yametumia mabomu ya mtawanyiko, katika shambulio jengine katika mji wa bandari ya Misrata, ambao umezingirwa na jeshi hilo.

Bandari ya Misrata.
Msimamizi wa bandari alisema mabomu hayo yaliripuka chini ya lori na kujeruhi watu wawili.
Mwandishi wa BBC mjini Tripoli anasema, waandishi wana picha ambazo zinaonesha wazi mabomu yaliyojizika ardhini, yaliyofyatuliwa kutoka kombora linalorusha mabomu mtawanyiko, ambayo yamepigwa marufuku katika nchi nyingi.

Juma lilopita NATO ilitegua mabomu yaliyolengwa dhidi ya meli katika pwani ya Misrata.
Na mizinga iliyofyatuliwa na jeshi la Gaddafi nchini Libya, inaarifiwa kuwa imepiga ardhi ya Tunisia kwenye mji wa Dehiba, ulio mpakani.
Vita baina ya jeshi la wapiganaji na jeshi la Kanali Gaddafi vimezidi kuwa vikali katika juma lilopita, kwenye milima ya magharibi mwa Libya.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni