Jumapili, 29 Mei 2011

NATO YASHAMBULIA LIBYA MCHANA TOFAUTI NA MAZOEA YAO YA KUSHAMBULIA USIKU.

NATO imeshambulia nyumba ya Gaddafi

NATO inasema kuwa imeangamiza minara ya walinzi katika eneo la nyumba ya Kanali Gaddafi wa Libya mjini Tripoli, kwa mashambulio mawili yaliyofanywa na ndege za umoja huo wa kijeshi.
Watu wakizungumza karibu na jumba la Gaddafi la Babu al_aziziya baada ya kushambuliwa mwezi Aprili
Waandishi wa habari mjini Tripoli, wanasema shambulio moja lilofanywa mchana, lilivunja sehemu za ukuta unaozunguka jengo la jeshi la Bab al-Aziziya.
Msemaji wa NATO, alieleza kuwa shambulio hilo ni funzo kubwa kwa kiongozi wa Libya, kwamba hawezi tena kujificha nyuma ya kuta ndefu

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni