Jumatatu, 15 Agosti 2011

CESC FABREGAS ATUA BARCELONA RASMI

Cesc Fabregas tayari ni mchezaji rasmi wa Barcelona baada ya kusaini mkataba wa miaka mitano na mabingwa hao wa Ulaya.
Cesc Fabregas
Cesc Fabregas


Nahodha huyo wa zamani wa Arsenal amefuzu uchunguzi wa afya yake aliofanyiwa mara mbili siku ya Jumatatu na atatambulishwa na klabu hiyo wakati wowote.
Arsenal itapokea kitita cha paundi milioni 30 na paundi milioni 5 nyingine zitatolewa kutegemeana na idadi ya mechi atakazocheza na vikombe itakavyoshinda Barcelona.
Siku ya Jumapili, Arsenal na Barca walithibitisha "kukubaliana kimsingi" juu ya kumuuza Fabregas.
"Tunaelewa hamu aliyonayo Cesc ya kurejea katika klabu ya nyumbani kwao na sasa ameafikiana na klabu ya Barcelona," alisema meneja wa Arsenal, Arsene Wenger.
"Tumekuwa tukifahamisha bayana hatukutaka Cesc aondoke na hali hiyo inasalia hivyo hivyo.
"Tunamshukuru Cesc kwa mchango wake katika klabu ya Arsenal na tunamuombea mafanikio huko aendako."
Barcelona imekuwa ikimuwinda Fabregas tangu msimu uliopita.
Cesc Fabregas
Cesc Fabregas

Taarifa za mpango wa kuuzwa kwa Fabregas zilithibitishwa wakati wa kipindi cha mapumziko kwenye mchezo wa awali wa kuwania Kombe la Hispania siku ya Jumapili, ambapo Barcelona ilitoka sare ya mabao 2-2 na Real Madrid.
Fabregas tayari ameshafanyia uchunguzi wa awali wa afya yake katika hospitali iitwayo Hospital de Barcelona.
Fabregas alifanya mazungumzo na wachezaji wenzake wa Arsenal kwa mara ya mwisho siku ya Ijumaa asubuhi na hakuwemo katika kikosi cha Wenger kilichocheza siku ya Jumamosi dhidi ya Newcastle katika mechi ya ufunguzi wa msimu ambapo timu hizo hazikufungana.
Hakuwemo katika ziara ya timu ya Arsenal barani Asia na pia hakucheza mechi nyingine za kujiandaa kwa msimu mpya wa ligi, zikiwemo mechi za Kombe la Emirates, kutokana na kusumbuliwa na maumivu ya msuli wa paja.
Fabregas
Fabregas

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Hispania, ameshaichezea nchi yake mechi 58 na kwa klabu ya Arsenal amecheza mechi 303 wakati wa kipindi cha miaka minane akiwa kaskazini mwa jiji la London na amefunga mabao 57 katika mashindano yote aliyocheza.
Mwezi wa Oktoba mwaka 2003, alikuwa mchezaji mwenye umri mdogo kuichezea Arsenal katika kikosi cha kwanza, ambapo mechi yake ya kwanza ilikuwa dhidi ya Rotherham United kuwania kufuzu kwa Kombe la Carling wakati huo akiwa na umri wa miaka 16 na siku 177.
Pia alikuwa mchezaji mwenye umri mdogo wa klabu hiyo kufunga bao, alipofunga wakati Arsenal ilipilaza Wolves mabao 5-1 mwezi wa Desemba mwaka huo wa 2003. Fabregas alikuwa katika kikosi cha Arsenal kilichoilaza Manchester United kwa mikwaju ya penalti na kushinda Kombe la FA mwaka 2005, na kuwa kombe muhimu la pekee aliloshinda na Arsenal kwa muda wote akichezea klabu hiyo.
Aliteuliwa kuwa nahodha wa Arsenal mwezi wa Novemba mwaka 2008. Mshambuliaji Robin van Persie anatazamiwa kuchukua nafasi ya unahodha wa kudumu wa Arsenal, ingawa hatacheza mechi dhidi ya Udinese baada ya kufungiwa kutokana na kadi nyekundu aliyooneshwa msimu uliopita walipocheza na Barcelona katika moja ya mechi za Ubingwa wa Ulaya.
Alipobanwa kuhusiana na mustakabali wa Fabregas na Samir Nasri - BBC ikifahamu fika naye yupo njiani kuelekea Manchester City -kwenye mkutano na waandishi wa habari siku ya Ijumaa, Wenger alisema anatumai "hakuna yeyote atakayeihama" Arsenal

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni