Jumapili, 21 Agosti 2011

DR. PETER KAMFUMU KUBEBA DHAMANA YA CCM UBUNGE WA IGUNGA TABORA.

Dr. Peter Kamfumu, kwa sasa ni Kamishna wa Madini Wizara ya Nishati na Madini, ndiye anayeongoza jahazi la CCM Igunga akijaribu kuvaa viatu vya Rostam Aziz.

KURA ZA MAONI CCM YAMPATA MRITHI WA ROSTAM IGUNGA , NI PETER KAMFUMU.

PETER KAMFUMU ameongoza kura za maoni za CCM zilizopigwa na Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM Wilaya ya Igunga Mkoani Tabora kwa ajili ya kuomba kugombea Ubunge Jimbo la Igunga lililoachwa wazi na Rostam Azizi aliyejiuzulu.

Taarifa iliyotua hivi punde katika mtandao huu kutoka radio Uhuru Fm inadai kuwa Ndugu KAMFUMU ambaye pia ni Kamishna wa Nishati katika Wizara ya Nishati na Madini amepata kura 588 kati ya kura 928 zilizopigwa na Wajumbe wa Mkutano huo katika uchaguzi uliofanyika jana Mjini Igunga.
Katibu wa CCM Wilaya ya Igunga Ndugu NEEMA ADAM ameiambia Uhuru FM kwa njia ya Simu kuwa jumla ya wanachama wa Chama Cha Mapinduzi Kumi na Tatu wamepigiwa kura za maoni katika mkutano huo.
Wanachama wengine waliopigiwa kura ni pamoja na Ndugu JAFARI ALI OMAR kura 163, SHAMSI FEROUZ IBRAHIMU kura 36, Ndugu HAMIS MAPINDA kura 36, Ndugu NGASA NIKOLAUS kura 18, Ndugu SELF HAMIS kura 13 na Ndugu SHIRE MASHAURI kura 16.

Wengine ni Ndugu HAMAD SAFARI kura 5, Ndugu MKOBA SHABAN kura 5 Ndugu DANIEL MBOJE kura 4, Ndugu ADAM KAMANI kura Tatu na Ndugu AMINA FUNDIKILA kura Saba.

Kulingana na Katibu huyo wa CCM Wilaya ya Igunga majina hayo yote yatapelekwa ngazi ya Mkoa ambayo nayo itayapitia na kisha kuyapeleka katika Kamati Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi kwa maamuzi zaidi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni