Jumamosi, 27 Agosti 2011

RAIS WA KENYA AWAFUKUZA KAZI BAADHI YA MAWAZIRI

Waziri ambaye ni mmoja ya watuhumiwa sita wakuu wa machafuko ya baada ya uchaguzi nchini Kenya Uliosababisha vifo vya zaidi ya watu 1,300 amefutwa kazi.
William Ruto

Rais Mwai Kibaki pia amemrudisha kazini Waziri wa Maswala ya nchi za njee aliyekuwa amesimamishwa kazi kufuatia tuhuma za ufisadi.
William Ruto ambaye ni mmoja ya washukiwa wakuu wa ghasia za baada ya uchaguzi nchini kenya, amefutwa kazi kama Waziri wa Elimu ya Juu.
Kufutwa kazi kwa Ruto kunakuja wakati Bwana Luis Moreno Ocampo akimsubiri huko The the Haegue kuanzia 1 September, 2011 ili uthibitishaji wa kesi inayomkabili kuhusu ghasia za zilizoikumba kenya mwaka 2008 ianze kusikilizwa.
Taarifa kutoka idara ya habari za rais pia zimesema kuwa waziri wa Afrika Mashariki profesa Hellen Sambili pia ametimuliwa. Ruto na Sambili wanatoka eneo la Rift Valley
Nafasi zao zimechukuliwa na wabunge wengine kutoka jimbo hilo hilo la Rift valley ,Prof. Margaret Kamar kama waziri mpya wa Elimu ya juu na Musa Sirma akiwa waziri mpya wa Afrika Mashariki.
Waziri Mkuu Raila Odinga

Wengine walifutwa kazi ni manaibu waziri wanne ambao wamekuwa ni wapambe wa William Ruto. Huku wakiasi chama chao cha ODM cha waziri Mkuu Raila Odinga na kukipigia debe chama kidogo cha UDM chenye ufuasi mkubwa eneo la Rift valley.
Na waziri wa Maswala ya nchi za Njee, Moses Wetangula ambaye alisimamishwa kazi karibu mwaka mmoja ulipita kutokana na kashfa ya kuuza majumba ya ubalozi wa Kenya nchini Japan amerudishwa kazini .
Kurudishwa kazini kwa Wetangula kumempa siku moja peke yake ya kujiandaa kabla ya kusafiri moja kwa moja hadi Addis Ababa, Ethiopia kuwakilisha Kenya katika mkutano wa kimataifa ulioandaliwa na Umoja wa Afrika kwa minajili ya kukusanya pesa za kusaidia kukabiliana na njaa katika upembe wa Afrika.
Lakini taarifa hiyo fupi haikusema kama uchunguzi uliokuwa ukiendelea kumhusu bwana Wetangula umekamilika na kumundolea lawama.
Taarifa hiyo inasema kuwa Rais Kibaki amefanya madadiliko hayo baada ya kushauriana na waziri Mkuu Raila Odinga.
Hata hivyo halmashauri ya kukabiliana na ufisadi nchini kenya imeeleza kusikitishwa kwake na hatua ya kumrudisha kazini bwana Wetangula. Tume hiyo imesema ilikuwa bado inamchunguza Waziri huyo

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni