Jumapili, 21 Agosti 2011

MAPIGANO NA WAASI WA LIBYA YAFIKA MJI MKUU WA TRIPOLI.


Baada ya saa kadha za milio ya bunduki katika mji mkuu wa Libya, Tripoli, Kanali Muammar Gaddafi na mwanawe wa kiume wamesisitiza kwamba wana hakika watawashinda wapiganaji.

Katika matangazo yao Kanali Gaddafi alisema, wafuasi wake mjini Tripoli wamewafyeka wale aliowaita "panya" walioingia mjini. Na katika hotuba nyengine, mwanawe, Saif Al-Islam Gaddafi, alikana kusallim amri.

Saif al-Islam Gaddafi alisema:

"Hili swala la kusalimu amri, au kupepea bendera nyeupe, siyo jambo ambalo mtu yeyote anafaa kulizungumza, kwa sababu limekataliwa.

Huo siyo uamuzi wa Muammar Gaddafi au Saif al-Islam; ni uamuzi wa watu wa Libya."

Saif al-Islam alisema ripoti za vyombo vya habari, kwamba Kanali Gaddafi na majeshi yake yanakaribia kushindwa, ni za uongo.

Viongozi wa wapiganaji wanasema wafuasi wao mjini Tripoli, wameanzisha harakati na wanashirikiana na wapiganaji wanaokaribia mji kutoka karibu pande zote

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni