Jumatano, 29 Juni 2011

VIGOGO ARDHI WAFIKISHWA MAHAKAMANI

Wednesday, June 29, 2011 12:10 PMVIGOGO nane wa Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi wakiwemo na Maofisa wa Ardhi wa Manispaa ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, wamefikishwa mahakamani kwa makosa ya kutumia madaraka wakwia kazini
Vigogo hao walifikishwa jana katika mahakama ya wilaya ya Kinondoni kwa
kosa la kuruhusu viwanja vya wazi vilivyopo ndani ya Manispaa hiyo kuvamiwa hali wakiwa kazini.

Mbele ya Hakimu Yohana Yongolo wa Mahakama hiyo watuhumiwa hao walisomewa mashitaka tofauti yaliyofikia 44 yote yakiwa kutumia madaraka vibaya.

Waliofikishwa mahakamanai akiwemo Ofisa Ardhi wa Manispaa ya Kinondoni Hamidu Mgaya, Anna Macha na Mapambano Baseka
Maofisa Mipango Miji wa Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi waliofikishwa mahakamani hapo ni Said Maligwah, Jumla Mmalala, Francis Woiso na Wanura Maranda.

Vilevile aliyekwua diwani wa Kata ya Kunduchi [ccm] Patrick Matoyola

Vigogo hao wamefikishwa mahakamani ikiwa ni ahadi ya Waziri ya husika kuwawajibisha wale wote waliohusika na kuza viwanja vya wazi ikiwa na wale wote waliosababisha uvamizi

Maoni 1 :