Jumapili, 26 Juni 2011

ATANGAZWA AMEFARIKI KUMBE KAZIMIA TU, DU! MADAKTARI MMESOMA LAKINI MMMH...!?

Atangazwa Amefariki, Azinduka Ndani ya Jeneza, Afariki Tena


Mwili wa Fagilyu Mukhametzyanov ukiwa umezungushwa kwenye kapeti baada ya kufariki kweli mara ya pili
Saturday, June 25, 2011 3:51 AMAlizunduka ghafla na kujikuta akiwa ndani ya jeneza watu wakiiaga maiti yake kabla ya kuzikwa, alikumbwa na mshtuko mkubwa baada ya kuambiwa kuwa madaktari walishaitangazia familia yake kuwa amefariki, kwa mshtuko huo alifariki kweli.
Wakati ndugu na jamaa huku wakiombeleza wakipita mbele ya jeneza lake ambalo liliachwa wazi kwa juu, Fagilyu Mukhametzyanov alizinduka na kuanza kupiga kelele baada ya kusikia watu wakisali kuiombea maiti yake iwekwe mahali pema peponi.

Fagilyu Mukhametzyanov mwenye umri wa miaka 49 wa mji wa Kazan nchini Urusi alitangazwa kimakosa na madaktari kuwa ameiaga dunia wakati alipokumbwa na shambulio la moyo nyumbani kwake na baadae kupoteza fahamu kabisa.

Mume wa Fagilyu, Fagili Mukhametzyanov, 51, aliambiwa na madaktari kuwa mkewe ameiaga dunia kutokana na shambulio la moyo.

Taratibu za mazishi zilianza na wakati watu wakiliaga jeneza, Fagilyu alizunduka ghafla na baada ya kugundua yuko ndani ya jeneza alipiga kelele.

Alikumbwa na mshtuko mkubwa uliopelekea apatwe na shambulio la moyo, aliwahishwa hospitali ambapo alilazwa kwenye chumba cha watu mahututi lakini safari hii aliweza kuishi kwa dakika 12 tu ndipo alipoiaga dunia kikweli kweli.

"Nina hasira sana na nataka majibu ya mambo yaliyojitokeza, hakuwa amefariki wakati alipotangazwa amefariki, wangeweza kuyaokoa maisha yake", alisema mumewe kwa hasira.

Msemaji wa hospitali, Minsalih Sahapov alisema kuwa wameanzisha uchunguzi kuhusiana na tukio hili

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni