Alhamisi, 16 Juni 2011

WANAFUNZI UDOM WASIMAMISHWA.

Jengo la Utawala Chuo Kikuu cha Dodoma

CHUO KIKUU cha Dodoma (UDOM) kimefungwa kufuatia kukithiri kwa vurugu zilizokuwa zikizifanywa na wanafunzi chuoni hapo.
Jana Uongozi wa chuo hicho kiliamuru wanafunzi kuondoka eneo la hilo kwa kuwapa masaa mawili wasionekanemaeneo ya chuo na kukitangaza kukifunga kwa kipindi kisichojulikana kuanzia jana.

Makamu Mkuu wa UDOM, Profesa Idris Kikula, alisema jana kuwa, uamuzi wa kukifunga chuo hicho una lengo la kuepusha baadhi ya wanafunzi na majanga yanayoweza kujitokeza kutokana na baadhi yao kukaidi amri ya kusimamisha mgomo wao uliodumu kwa muda mrefu chuoni hapo.

Kikula amesema uamuzi huo umekuja baada ya wanafunzi wa mwaka wa pili na wa tatu wanaochukua kozi ya Sayansi ya Jamii kuilazimisha Serikali kuwapa posho za mazoezi kwa vitendo kabala ya muda.

Amefafanua kuwa, wanafunzi hao wanatakiwa waende kwenye mafunzo kwa vitendo katikati ya mwezi ujao na walishakubalina kuwapa posho hizo lakinis wanafunzi hao wametishia mgomo kuilazimisha Serikali kuwapa posho hizo kwa sasa.

Mgomo huo umesababisha wanafunzi wapatao 400 kusimamishwa masomo na kufuatia hali hiyo Profesa Kikula amesema watachapisha majina ya watakaotakiwa kurudi chuoni katika tovuti ya chuo

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni