Jumatatu, 27 Juni 2011

AFUKUA MAITI YA MUMEWE

Ukistaajabu ya Musa...



Maiti ya Keneth ikifukuliwa ili ivalishwe meno ya bandia aliyokuwa akiyatumia enzi za uhai wake Sunday, June 26, 2011 3:22 AM
Mwanamke mmoja wa nchini Marekani ameifukua maiti ya mumewe toka kaburini kwasababu maiti hiyo ilizikwa huku mumewe akiwa amevalishwa meno ya bandia ambayo yalikuwa si ya kwake.
Phyllis Manis hakutaka mumewe apumzike kaburini huku akiwa amevalishwa meno ya bandia ambayo si ya kwake.

Phylis aliifukua maiti ya mumewe, Keneth iliyokuwa imezikwa kwenye makaburi ya Chattanooga, Tennessee ili aweze kumvalisha meno ya bandia aliyokuwa akivaa kila siku.

Televisheni ya WTVC ya Marekani iliripoti kwamba, wakati Keneth alipokuwa amelazwa hospitali kwenye chumba cha watu mahututi, madaktari waliyachanganya meno yake ya bandia na meno ya bandia ya mtu mwingine hali iliyopelekea Keneth avalishwe meno ya bandia ya mtu mwingine.

Baada ya mazishi ya Keneth ambaye alifariki akiwa na umri wa miaka 76, Phylis aligundua waleti na funguo za mgonjwa aliyekuwa amelazwa chumba kimoja na Keneth zikiwa zimechanganywa na baadhi ya vitu vya Keneth yakiwemo meno ya bandia aliyokuwa akiyavaa Keneth enzi za uhai wake.

"Mume wangu amelala kaburini akiwa na meno ya bandia ya mtu mwingine, siwezi kuruhusu hali hii itokee kwani najua yeye mwenyewe asingependa iwe hivyo", alisema Phylis alipokuwa akihojiwa na televisheni ya WTVC.

Msemaji wa hospitali ya Parkridge Medical Centre ambako tukio hilo lilitokea alisema kwamba hospitali inaomba radhi na imekubali kulipa gharama za kuifukua maiti ya Keneth pamoja na kumnunulia meno mapya mgonjwa ambaye meno yake ya bandia alivalishwa Keneth kimakosa.

"Najua sasa mume wangu atapumzika vizuri na pia familia yetu itaweza kupumzika", alisema Phylis baaada ya maiti ya mumewe kufukuliwa ili kuvalishwa meno ya bandia aliyokuwa akiyavaa enzi za uhai wake.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni