Alhamisi, 23 Juni 2011

WACHUNGAJI WA NIGERIA WANA UTAJIRI MKUBWA KAMA WAFANYABIASHARA YA MAFUTA.

Mchungaji Gwajima wa Tanzania

Mchungaji Getrude Rwakatare wa Tanzania
Wahubiri wa Nigeria wamefanikiwa katika miradi yao na kuwa na utajiri unaolinganishwa na matajiri wanaofanya biashara ya mafuta.
Kwa mujibu wa muandishi wa blogu moja huko Nigeria aliyefanya utafiti wa wahubiri hawa wa neno la Mungu ameiambia BBC kuwa wana Biashara kabambe utadhani wana visima vya mafuta.
Waumini wakibarikiwa

Mhubiri afaidi baraka zake

Mfonobong Nsehe, mwandishi wa blogu ya jarida la kibiashara la Forbes anasema kuwa ma- pastor wanamiliki biashara kubwa kuanzia hoteli kubwa hadi biashara za chakula, mfano wa vyakula vya haraka kama vile 'nyama na kuku'' sawa na Kentucky' ambazo ni vivutio kwa familia na vijana.
Mwandishi huyu anasema kuwa"Uhubiri ni biashara kubwa. Faida yake ni sawa na biashara ya mafuta ya petroli.
visima vya mafuta
Kituo cha Mafuta.

Alitoa mfano wa utajiri wa Wahubiri watano ambao wana takriban dola milioni 200m.
Kanisa za wahubiri wa aina hii zimeimarika nchini Nigeria katika miaka ya hivi karibuni, ambapo maelfu kwa maelfu wameshiriki na kujiunga nazo.
Bw.Nsehe anasema Mhubiri anayeongoza kwa utajiri, Bishop David Oyedepo wa Kanisa lijulikanalo kama Living Faith World Outreach Ministry, alikadiriwa kuwa na utajiri wa takriban dola milioni150.
Bishop Oyedepo anamiliki kampuni ya kuchapisha, Chuo kikuu, shule moja ya msingi ya kifahari, ndege zake nne za binafsi za kifahari na nyumba kadhaa mjini London na Marekani.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni