Jumapili, 5 Juni 2011

MBOWE ASWEKWA LUPANGO, KUSAFIRISHWA HADI ARUSHA AKAJIBU MASHTAKA.

Mh.Freeman Mbowe
 

Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Bw. Freeman Mbowe amekamatwa na jeshi la Polisi mkoani Dar es salaam kufuatia agizo la pili la Hakimu wa Mahama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Arusha baada ya kushindwa kujisalimisha mahakamani katika kesi inayomkabili ya kufanya kusanyiko usio halali mkoani Arusha tarehe 5 Januari 2011. Mbowe alikamatwa jana jijini Dar es Salaam wakati alipokwenda kujisalimisha katika kituo Kikuu cha Polisi. Habari zinasema kuwa Mbowe amelala Rumande na atasafirishwa kwenda Mjini Arusha kujibu shtaka linalomkabili. Polisi wameimarisha ulinzi katika kituo hicho

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni