Jumanne, 21 Juni 2011

MASHOGA WARUHUSIWA KUWA MAKASISI UINGEREZA, DUNIA INAELEKEA KUBAYA AU!?

Mashoga Kuwa Mapadri Uingereza


Mchungaji ambaye pia ni shoga, Dr Jeffrey John
Jumuiya makanisa ya Anglikana, Uingereza inatarajiwa kutangaza rasmi kuwa wanaume waliojitangaza wazi kuwa wao ni mashoga wataruhusiwa kuwa mapadri iwapo watatimiza sharti la kujizuia kufanya ngono
Taarifa rasmi ya kuruhusu mashoga kuwa mapadri inatarajiwa kutolewa jumatatu ambapo imetangazwa kuwa ni katika kuondoa ubaguzi katika masuala ya dini bila ya kuwabagua watu kwa tabia au matendo yao kinyume na maumbile.

Sharti la kuwataka mashoga wajizuie kufanya ngono iwapo wanatakiwa kupewa nafasi hiyo kubwa ya kidini huenda ikasababisha mtafaruku kwani mchungaji mmoja shoga anapinga sharti hilo na anatishia kujitoa yeye na wafuasi wake duniani toka kwenye kanisa hilo.

Mwaka 2003, mchungaji ambaye pia ni shoga na mwanaharakati wa kutetea haki za mashoga, Dr Jeffrey John alitajwa jina lake miongoni mwa wagombea wa uaskofu wa mji wa Reading hali iliyosababisha mtafaruku mkubwa kwenye kanisa la Anglikana na kupelekea aamue kulitoa jina lake.

Kanisa la Anglikana halitaki mgogoro wowote utokee na kuwagawa waumini wa kanisa hilo duniani.

Hata hivyo, baadhi wa waumini wa kanisa hilo la Anglikana wanapinga uamuzi wa kuruhusu mashoga kuwa mapadri kwani ni kinyume na mafundisho ya kanisa

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni