Jumanne, 7 Juni 2011

KASHFA KWA WATEULE WA KENYA MHIMILI WA MAHAKAMA.

Mutunga: Sishiriki mapenzi na wanaume

Willy
Dk Willy Mutunga

Jaji mkuu mteule nchini Kenya Dk Willy Mutuga amekanusha kama anashiriki mapenzi ya jinsia moja.
Mutunga aliyasema hayo alipokuwa anahojiwa na kamati maalum ya bunge.
Kamati hiyo ya bunge ilifanya vikao vyake vya siku mbili kusikia shutuma zilizotolewa dhidi ya walioteuliwa kuchukua nyadhifa za jaji mkuu,naibu jaji mkuu na mwendesha mashtaka mkuu.

Anashiriki

Hatua hii ilichukuliwa baada ya baadhi ya watu na hasa makanisa yakidai walioteuliwa si watu wanaozingatia maadili ya kifamilia kukiwemo na shutuma kuvaa hereni kwenye sikio la kushoto kwa Dk Mutunga ni ishara kwamba anashiriki mapenzi ya jinsia moja.
"Sishiriki mapenzi na wanaume,ila siwezi kuwabagua wanaume au wanawake wanaoshiriki mapenzi hayo,mimi mwenyewe mpwa wangu ni wa jamii hio",alisema Dk Mutunga.

Mchakato

Naibu jaji mkuu mteule Nancy Baraza pia alikuwa na muda wake wa kujitetea,alipoulizwa kwa nini alikita utafiti wake wa shahada ya uzamifu katika suala la haki za wapenzi wa jinsia moja.
Baraza alisema anafanya hivyo kwa kuwa alitaka kuwa mbunifu na kufanya utafiti wa kipekee ambao haujawahi kufanywa nchini Kenya.
Baada ya vikao hivyo kwa uma ambavyo vimetumika kuwatathmini tena wateule,majina hayo yatawasilishwa bungeni kwa ajili ya kupigiwa kura,ikiwa wataidhinishwa basi watachukuwa nyadhifa na iwapo watakataliwa bai mchakato wa usaili utaanza upya

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni