Jumanne, 14 Juni 2011

MMOJA AUAWA KATIKA UPORAJI MUHIMBILI JANA.



Sabina Masawe aliyejeruhiwa kwa kupigwa risasi mguu wa kushoto na majambazi Muhimbili akiwa wodini kwa matibabu Tuesday, June 14, 2011 12:08 PM
TUKIO la uporaji fedha lililotokea jana mapema katika Hospitali ya Taifa Muhimbili umesababisha upotevu wa shilingi milioni kumi na mbili na laki saba ambazo ziliporwa na majambazi waliovamia hospitalini hapo
Tathimini hiyo imetolewa jana na Afisa Uhusiano wa hospitali hiyo, Bw.Eminael Eligaesha

Eligaesha amesema kuwa, katika tukio hilo jumla ya shilingi million kumi na mbili na laki saba ndizo ziliibiwa katika tukio hilo kwa wahasibu wa hospitalini hapo”CashCollecter” walivamiwa na majambazi hayo na kuporwa mkoba uliokuwa na fedha hizo

Alisema wakusanyaji fedha hao walikuwa wakitumia gari aina ya Pickup walikuwa wakikusanya fedha katika vitengo hospitlaini hapo na walipokuwa wakitoka jengo la OPD kwenda jengo la Uhasibu ghafla walivamiwa na kuzingirwa na watu wapatao sita na walimpiga risasi askari aliyekuwa na watumshi hao na mwingine alijeruhiwa wakati akishuka katika gari hilo na hawakuweza kujitetea na walinyanganywa fedha hizo

Alisema askari huyo alifariki dunia majira ya saa 3 usiku jana katika hospitali hiyo na Bi. Sabina Masawe alijeruhiwa kwa kupigwa risasi katika paja la kushoto na anaendelea na matibabu hospitalini hapo kubaini kama risasi ipo mwilini ama ilitoka

Maoni 1 :