Jumanne, 28 Juni 2011

WALOKAMATWA NA MAMILIONI YA DOLA SOMALIA WAACHIWA

..Wabeba kikombozi wasamehewa
Wakuu wa Somalia wamewasamehe wageni 6 waliokutikana na hatia ya kuingiza nchini dola milioni-tatu, ili kuwalipa maharamia kikombozi.

Harmia la kisomali


Msemaji wa serikali ya mpito, Abdirahman Osman Yarisow alieleza wanaume hao, kutoka Uingereza, Marekani na Kenya waliachiliwa huru kwa sababu ya kuwaonea huruma.

Alisema kikombozi walichokuja nacho kimetaifishwa na serikali.

Juma lilopita, wanaume hao walihukumiwa kifungo cha miaka 15.

Washtakiwa hao walikamatwa mwezi uliopita punde baada ya kutua kwenye uwanja wa ndege mjini Mogadishu.

Watu hao walifanyiwa kesi ya faragha kwenye uwanja wa ndege ambako walitua mwezi uliopita.

Inasemekana walipowasili Mogadishu walikuwa wamebeba mamilioni ya dola kama kikombozi.

Msimamo rasmi wa serikali ya Somalia ni kuwa inapinga kulipa kikombozi lakini tabia hiyo imekuwa ni kawaida sasa.

Umoja wa mataifa unakisia zaidi ya dola milioni moja zililipwa kwa maharamia wa Somalia mwaka jana

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni