Alhamisi, 16 Juni 2011

BAJETI YA UPINZANI YASIFIWA.

Waziri kivuli wa fedha Zitto Kabwe.

Upinzani Bungeni, imesomwa jana na Waziri Kivuli wa Fedha na Uchumi, Bw. Kabwe Zitto na kuonekana kuwa na tofauati kubwa na ile iiyowasilishwa na Waziri Mustapha Mkulo
Hotuba hiyo ilitoa mapendekezo mfumo mzima wa kulipana posho za vikao uondoke katika utumishi wa umma na ziruhusiwe posho za kujikimu kama viongozi au watumishi wakiwemo na maafisa wa umma wanaposafiri nje ya vituo vyao vya kazi.

Kupinga posho za vikao zifutwe mara moja kwa kuwa hazina msingi wowote ni kuiongezea mzigo serikali.

Akifafanua kuhusu posho hizo “ Sisi tulipwe posho za vikao ikiwa ni sehemu la jukumu, mbona polisi halipwi posho kwa kulinda, mwalimu halipwi posho kwa kuingia darasani na mbona nesi halipwi posho kwa kusafisha vidonda vya wagonjwa? Hiisi sahihi zifutwe mara moja? Alisema Kabwe...

Imependekeza kubana kampuni kubwa kulipa kodi inavyostahili, imetoa maoni ya kufutwa kabisa kwa msamaha wa kodi kwenye mafuta kwa kampuni za madini na zile za ujenzi, kwani unasababisha upotevu mkubwa fedha za umma.

Pia imependekeza elimu ya bure kwa Watanzania kuondoa ada za shule za sekondari na kupiga mnada magari ya anasa ya serikali yalipo sasa.

Hotuba hiyo imesema kulifufua Shirika la Ndege (ATCL), ambapo Mashirika ya Umma mengine kama Ngorongoro Conservation Area Authority (NCAA) na TANAPA.

Kuboresha sekta nzima ya madini na kufafanua ikisimamiwa vizuri ipasavyo pato linaongezeka kampuni za madini zingewekeza kwenye migodi serilkali itapata faida a fedha kutoka huko kwani mauzo ya dhahabu huishia kulipia madeni na riba hivyo kukosesha serikali mapato

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni