Jumatatu, 13 Juni 2011

MAJAMBAZI YAVAMIA HOSPITALI YA MUHIMBILI NA KUPORA FEDHA.


Kundi la majambazi wasiofahamika idadi yao wamevamia sehemu ya mapokezi katika Hospitali ya Taifa Muhimbili na kufanikiwa kupora fuko la fedha ambapo haijafahamika mara moja kulikuwa na kiasi gani cha fedha
Uvamizi huo ulitokea asubuhi ya leo na kufanikiwa kumjeruhi askari na mtu mmoja aliyekuwa akihusika na ukusanyaji wa fedha katika vitengo hivyo

Imedaiwa leo wakusanyaji mapato hospitalini hapo walianza kukusanya mapato ya hospitalini hapo na ghafla walipofika eneo hilo walivamiwa na majambazi hayo na kufanikiwa kupora fedha

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni