Alhamisi, 16 Juni 2011

DROGBA APATA JIKO,BAADA YA MUDA MREFU KULA MAGENGENI.

Hatimaye Drogba Aoa


Drogba na mkewe Lalla Diakite
Baada ya kuishi na mpenzi wake kwa muda mrefu, nyota wa soka wa Chelsea na Ivory Coast, Didier Drogba amefunga pingu ya maisha na mpenzi wake katika harusi ya kukata na shoka ambayo masupastaa wa R&B, wacheza soka na nyota wa NBA walihudhuria.
Mfumania nyavu wa Chelsea, Didier Drogba ameamua kumuoa mpenzi wake wa muda mrefu ambaye amezaa naye watoto watatu kwa kufunga ndoa ambayo sherehe yake ilihudhuriwa na masupastaa mbalimbali.

Drogba mwenye umri wa miaka 33, alifunga ndoa na mama watoto wake, Lalla Diakite mjini Monaco, Ufaransa.

Mmiliki wa Chelsea, bilionea Roman Abramovich ndiye aliyeiongoza harusi hiyo huku Salomon Kalou na Florent Malouda wakiwa wapambe wa bwana harusi.

Nyota wa RnB, Akon na masupastaa wa mpira wa kikapu wa NBA walikuwa miongoni mwa wageni waalikwa katika harusi hiyo.

Fally Ipupa toka Jamhuri ya Kongo naye alikuwepo kwenye harusi hiyo sambamba na nyota wa muziki wa Nigeria, J Martins ambaye alipewa usafiri wa bure na Drogba ili aweze kupafomu na Ipupa wimbo wake wa Jupa Remix.

Michael Essien naye alitia maguu kwenye harusi hiyo baada ya kupanda pipa toka Nigeria ambako alishiriki mechi maalumu pamoja na mastaa mbalimbali wa soka duniani kumuaga rasmi Nwako Kanu ambaye amestaafu soka rasmi baada ya miaka 16 ya kulisakaka kabumbu kimataifa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni