Jumapili, 12 Juni 2011

MICHUANO YA CAF AFRIKA; SIMBA SC YAICHAPA MOTEMA PEMBE BAO 1-0

Shirikisho linaloongoza mchezo wa mpira wa miguu CAF linasema kuwa Libya bado ndiyo iliyopangiwa kuandaa Kombe la Mataifa ya Afrika mwaka 2013.
Hata hivyo Caf linasema kuwa mipango mbadala ipo ikiwa Libya itashindwa kutokana na ghasia za sasa hivi nchini humo.
Waasi wanaotaka kumpindua Kanali Mummar Gaddafi wanadhibiti sehemu kubwa ya mashariki ya nchi hiyo.
Katibu mkuu wa CAF Hicham El Amrani ameiambia BBC kuwa mashindano yote ambayo Libya ilikubali kuandaa siyo tu Kombe la Mataifa ya Afrika bali hata mashindano ya wachezaji wanaocheza soka katika vilabu vya nyumbani CHAN na Futsal bado tunaonelea kuwa ni jukumu la Libya.
Libya iliahidi kuandaa
Mipango mingine ipo

Katika kinyanganyioro cha vilabu klabu ya JS Kabylie imekuwa ya kwanza kufuzu kwa hatua za makundi katika Kombe la shirikisho kwa ushindi wa 2-0 dhidi ya ASC Jaraaf ya Senegal mechi iliyochezwa ijumaa mjini Tizi Ouzou.
J.S KABYLIE
Mshambuliaji wa Kabylie

Mabao ya Kabylie yalitiwa kimyani na beki Chemseddine Nessakh na kiungo Saad Tedjar kutimiza jumla ya mabao 3-1 kwa klabu hiyo ya Algeria.
Ikumbukwe kuwa klabu hiyo JS Kabylie ilikuwa bingwa wa Afrika mwaka 1981 na 1990.
Wakati huo huo Kufuatia ushindi wa Asec Mimosas ya Ivory Coast wa 4-0 dhidi ya Primeiro Agosto ya Angola katika mchuano wa kwanza na kutoka sare ya 1 1 katika mecghi ya marudiano nchini Angola, Asec Mimosa inapiga hatua kwa ushindi wa jumla ya bao 5-1 il hali Primeiro itabidi isubiri msimu ujao.
Wakati Primeiro ya Angola ikisubiri fursa ya kushiriki michuano ya Afrika mwakani, watani wao Inter Clube ilisababisha sare ya 2-2 ugenini Morocco dhidi ya klabu ya nchini humo Difaa al Jadida, mechi ya kwanza mjini Luanda ilimalizika kwa Difaa kudundwa matatu kwa bwerere.
Entente Setif ya Algeria ilikuwa nchini Nigeria kuchuana na Kaduna united baada ya ushindi wa 1-0 nchini Algeria tunasubiri matokeo ya mchuano wa mjini Kaduna leo.
mgogoro nchioni Libya
CAF inatafakari mwenyeji mwingine

Na mgogoro wa Libya umeanza kuathiri ratiba ambapo mechi kati ya Sunshine stars ya NIGERIA na Al Ittihad ya Libya ilibadilishwa ifanyike kwa mkondo mmoja badala yua miwili ikitazamiwa kuchezwa kati ya tareh 10 na 12 juni yaani leo
Huko Fez nchini Morocco,l Zesco united ya Zambia ilikuwa uwanjani kwa matumaini ya kuongezea ushindi wao wa bao moja kwa sufuri majuma mawili mjini Lusaka lakini waligutushwa kwa bao mbili za Maghreb Fez na hivyo Fez inapiga hatua kwa ushindi wa 2-1.
Mjini Dar es Salaam Tanzania Simba ya Dar es Salaam illipokea klabu ijulikanayo kama Darling Club Motema Pembe kutoka Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo.
Simba Sports au mnyama kama wapenzi wake wanavyopenda kumuita alimtafuna Motema Pembe 1-0 bao lililotiwa kimiani na mshambuliaji Mussa Hassan Mgosi.
Licha ya ushindi huo Simba ina kibarua itakapochuana na Motema Pembe katika mechi ya marudiano mjini Kinshasa jumapili ijayo. Ina maana Simba haitoweza kupumzika.
Kwa upande mwingine mjini Nairobi Sofapaka iliwapa matumaini mashabiki wake licha ya kuingia uwanjani ikiwa na deni la bao 3-0 katika mechi ya kwanza dhidi ya Club Africain majuma mawili yaliyopita.
Sofapaka ilitumia vizuri uwanja wa nyumbani na kuisukuma Club Africain na kupata magoli matatu ingawa Africain iliweza kufunga bao moja la ugenini.
Bao hilo la ugenini la Africain ndiyo lililoiondoa Sofapaka na kuhitimisha safari yake.

Maoni 1 :