Alhamisi, 23 Juni 2011

KOCHA MPYA CHELSEA

Villas-Boas kuwa kocha mpya wa Chelsea

Andre Villas-Boas atakuwa meneja mpya wa Chelsea, BBC inafahamu.
Andre Villas-Boas
Andre Villas-Boas akisherekea na wachezaji wa FC Porto Ushindi wao

Alijiuzulu kutoka timu ya Porto siku ya Jumanne baada ya kuisaidia kushinda ligi za Ureno na ligi ya Europa msimu uliopita.
Porto imepokea malipo ya pauni za Uingereza milioni £13.3m kiwango ambacho kipo kwenye mkataba wa Villas-Boas,kutoa nafasi kwa yeye kuondoka.
Chelsea, ambayo imemfuta kazi Carlo Ancelotti mwezi Mei, wameeleza nia yao na tayari wanajadiliana masuala ya mkataba na kocha huyo mwenye umri wa miaka 33.

Chelsea kujadili mkataba na Villas-Boas

Roman Abramovich
Mmiliki wa Chelsea Roman Abramovich
" Tunatarajia kukubaliana naye juu ya masuala binafsi ya mkataba na kutoa tangazo rasmi baadaye,"taarifa kutoka kwa timu ya Chelsea ilisema.
Katika taarifa kutoka Porto, timu ya Urenoi inasema kuwa nafasi ya Villas-Boas imechukuliwa na naibu wake Vitor Pereira,ambaye alitia saini mkataba wa misimu miwili.
Rais wa Porto Jorge Pinto da Costa amesema kuwa hajashangazwa na kuondoka kwa Villas-Boas na kusema: " ''Alipokwenda kwa mapumziko ya wikiendi London mwezi mmoja uliopita,nilizungumza na Vitor Pereira na nikamuuliza kama atakuwa tayari kuchukua nafasi hio.Akaniambia yuko tayari na hapo nikaridhika.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni