Ijumaa, 25 Novemba 2011

HAKIMU AWAWAKIA MAWAKILI WASOFIKA MAHAKAMANI KUWA ATAPAMBANA NAO.

Aliyekuwa Mhasibu TRA -Justice Katiti
HAKIMU Mkazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Waliyalwande Lema ametangaza mgogoro na mawakili wa washitakiwa katika kesi ya ya wizi wa Sh bilioni 3.8 inayomkabili mhasibu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Justice Katiti na wenzake wanne.


Kesi hiyo Novemba 24 ilikuja kwa ajili ya kutajwa na kupangiwa tarehe ya kuendelea kusikilizwa, ndipo Lema alipotangaza kuwa atafanya ukorofi kwa wakili ambaye hatafika mahakamani katika tarehe ambazo atakuwa amepanga kusikiliza kesi hiyo.


Lema alitoa onyo kwa mawakili hao kuwa wasipofika mahakamani siku hizo hatasimamisha usikilizwaji au kuahirisha kesi, hivyo wawepo vinginevyo atafanya ukorofi na ametoa taarifa mapema.


“Kawaelezeni mawakili wenzenu, yule pasua kichwa ametangaza ukorofi, sitaki kuandika tu kwenye jalada hapa nasema kabisa asiyefika mahakamani, mimi nitaendelea na kesi na mteja wake atakuwa hana mwakilishi,” alisema Lema.


Lema alisema kifo tu au ugonjwa ndivyo vitakavyomfanya asisikilize kesi hiyo, lakini si mawakili wa washitakiwa kutokuwepo mahakamani katika siku hizo ambazo ni kuanzia Desemba 6 hadi 8, mwaka huu.


Katika mashtaka yao wanadaiwa Mei na Novemba mwaka 2008 jijini Dar es Salaam walikula njama ya kuiba Sh bilioni 3.8 za TRA na kuzihamishia kwenye akaunti za kampuni mbalimbali na za watu binafsi

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni