Alhamisi, 3 Novemba 2011

DAKTARI TEMEKE AUAWA




DAKTARI MKUU MSAIDIZI wa Hospitali ya Temeke ya jijini Dar es Salaam, Kassim Kateta [43] ameuawa na watu wanadaiwa kuwa ni majambazi usiku wa jana
Kateta alifariki jana usiku majira ya saa 3 akiwa katika duka lake la kuza madawa linalotambulika kwa jina la Kotindi Pharmas lililopo jirani na hospitali hiyo

Kamanda wa Polisi Mkoa waTemeke, David Missime amesema kuwa, watu wawili ambao hadi sasa hawajafahamika ni akina nani walimvamia daktari huyo dukani kwake na kumuamuru atoe fedha na vitu vingine vya thamani

Kamanda huyo amesema kuwa ,kabla daktari huyo hajafanya chochote mmoja wao kati ya watu hao alimfyatulia risasi ya kifua daktari huyo na kutokea mgongoni kisha wao kutoweka na gari la daktari huyo

Kamanda huyo amesema jeshi hilo linafanya juhudi za kuwasaka watu hao pamoja na kuchunguza chanzo cha mauaji hayo ambacho hadi sasa haijafahamika

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni