Jumanne, 20 Septemba 2011

VIONGOZI WA CHADEMA WAWATETEA WAFUASI WAO WALIOMDHIBITI MKUU WA WILAYA YA IGUNGA KUWA WALIKUWA SAHIHI.!!!!!!

Mh. Tundu Lissu akiongea na Waandishi wa habari jana huko Igunga akilaani kitendo cha Wabunge wawili na mfuasi mmoja wa CHADEMA kufikishwa mahakamani Tabora juzi kwa kosa la kumshambulia Mkuu wa Wilaya ya Igunga aliyedaiwa kuingilia mkutano wao wa kampeni, alitaja pia nia yao ya kufanya lolote linalowezekana ili washinde kesi hiyo. Alisema watuhumiwa hao hawana kosa lolote walilotenda zaidi walikuwa wanalinda maslahi ya Chama chao.

Hivi ndio mambo yalivyokuwa hadi kupelekea Lissu kutetea waliopelekwa mahakamani, haya tusubiri tuone mahakama ikionesha haki imetendeka. Nasikia Lissu nae ni mwanasheria.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni