Jumatano, 14 Septemba 2011

JAMAA AKOJOA MAHAKAMANI, HAKIMU ASHANGAA.


NewsImages/5949810.jpg
Wednesday, September 14, 2011 2:07 AMDalili za kesi kwenda vibaya zilianza kuonekana pale mshtakiwa mmoja wa nchini Marekani alipoamua kukojoa mahakamani na kumfanya hakimu amuambie 'Sijui ulivyolelewa, unaonyesha tabia mbaya mahakamani'.
Kijana mweusi mwenye umri wa miaka 17 wa nchini Marekani alimuudhi hakimu pale alipoamua kusaula nguo zake na kukojoa mahakamani mbele ya umati wa watu waliokuwepo mahakamani kusikiliza kesi hiyo.

Kijana huyo aliyetajwa kwa jina la Corey Webb alifikishwa mahakamani kwa kumpiga risasi afisa wa polisi wakati alipokuwa akiwazuia kutoroka toka kwenye jela ya watoto.

Webb kabla ya kuamua kukojoa mahakamani alikuwa akifanya vituko mbali mbali kama vile kupiga kelele wakati akisomewa mashtaka yake. Aliwashangaza watu alipomtaka hakimu amfukuze wakili aliyekuwa akimtetea.

"Sijui umelelewaje lakini kukojoa kwenye pipa la taka ndani ya mahakama ni tabia mbaya", alisema jaji huyo baada ya Webb kuteremsha nguo zake na kukojoa ndani ya mahakama.

Kesi iliahirishwa hadi siku nyingine

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni