Jumamosi, 17 Septemba 2011

TIZAMA JINSI DC ALIVYODHALILISHWA NA WATU WANAOSEMEKANA NI CHADEMA, KAMA KWELI HIVI HAO CHADEMA NI NANI NCHI HII HADI WAACHWE WANAFANYA HAYA!!!?

DC wa Igunga Bi. Kimario akiwa na masikitiko makubwa baada ya kushambuliwa na wafuasi wa CHADEMA juzi.

Hivi hawa jamaa wana akili kweli!!? Mkutano wa Ndani wa kiutendaji wa kiongozi wa serikali unawezaje kuathiri Mkutano wa Hadhara wa kampeni. Hapa Mkuu wa Wilaya akitolewa nje toka Ukumbi wa Mikutano, sasa utasemaje kakuingilia kwenye Mkutano wako ikiwa wewe unafanyia nje na wenzio ndani!? Tujifunze siasa za kuvumiliana, hapa sio Libya kwa Wapinzani wasio na staa na viongozi wao hata kama wamewafanyia mazuri, Hawa wachukuliwe hatua kali, haki za binadamu ni lazima zifuatwe, mwanaume unamkamata vipi mwanamke maungoni? Vyombo vya Dola viwajibike hasa kwa hili.

Ubabe mtupu, hapa Diwani wa CCM naye katiwa nguvuni na dola ya Chadema, ni maoni yangu tu na uchambuzi tu, siegemei chama chochote lakini udhalilishaji huu siukubali hata siku moja kwa kulinda heshima ya nchi hii na miaka hamsini ya Uhuru, haikubaliki.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni