Jumapili, 31 Julai 2011

TEKNOLJIA YA KAMERA KATIKA GOLI KUANZA KUTUMIKA.

Teknolojia katika soka

Teknolojia  katika soka
Teknolojia katika soka
Teknolojia ya kutumia kamera katika goli huenda ikaanza kutumika katika ligi kuu ya Premier mwanzoni mwa msimu ujao wa 2012-13.
Halmashauri ya kimataifa ya chama cha mpira cha England itatoa uamuzi kama idhinishe mfumo huo ama la mnamo mwezi wa Machi 2012.
Ikiwa itathibitishwa basi kiongozi wa FIFA Sepp Blatter anasema ligi za soka zitaweza kuutumia mwanzoni mwa msimu wa 2012-13 endapo utakua hauna kasoro wala hautagharimu fedha nyingi.
Mkuu wa ligi ya Premier ya England, Richard Scudamore amesema kwamba watautumia mfumo huo mara tu utakapoidhinishwa.

Teknolojia ya goli kuidhinishwa.
Blatter aliongeza kusema kwamba teknolojia hiyo inaweza pia kutumika katika michuano ijayo ya kombe la dunia la mwaka 2014 nchini Brazil .
Kwa miaka mingi mkuu huyo wa Fifa amekua akipinga matumizi ya teknolojia katika eneo la goli lakini inaelekea alibadili mawazo yake baada ya mabishano makali kuzuka mnamo mwaka 2010.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni