Jumatano, 20 Aprili 2011

MAN-U YAKABWA KOO

Manchester yabanwa na Newcastle

Manchester United imebanwa na Newcastle kwenye uwanja wa St James Park na hivyo kutoa matumaini kwa Arsenal na Chelsea katika kuwania ubingwa.
Newcastle
Newcastle

United inaongoza msimamo wa ligi ikiwa na pointi 70 ikiwa imesalia michezo mitano.
Javier Hernandez na Wayne Rooney walikosa nafasi nzuri walipobaki na kipa, lakini Ryan Giggs alikosa bao kwa kupiga mkwaju wake nje.
Stephen Ireland angeweza kuipatia ushindi Newcastle, lakini mkwaju wake pia ulitoka nje.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni