Ijumaa, 30 Desemba 2011

MBUNGE ASEMA RAIS MUGABE NI SHOGA.

Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe.
Mbunge wa chama cha MDC (Movement for Democratic Change) cha nchini Zimbabwe amejikuta akiingia matatani baada ya kudai rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe alifanya mapenzi ya jinsia moja.Mbunge huyo ametupwa jela kwa siku saba.

Mbunge huyo wa kike aliyetajwa kwa jina la Lynette Kareny alisema kuwa Robert Mugabe ambaye pia ni rais wa chama tawala cha Zanu-PF alifanya mapenzi na wanasiasa wawili wa kiume.

"Karenyi anatuhumiwa kutoa kauli hiyo ya kumkashifu kiongozi wa nchi wakati wa mkutano wa hadhara wa chama cha MDC uliofanyika disemba 9 kwenye viwanja vya mpira vya Chimanimani,” limeripoti gazeti la The Herald la nchini Zimbabwe

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni