Ijumaa, 9 Desemba 2011

PONGEZI WATANZANIA KWA KUADHIMISHA MIAKA HAMSINI YA UHURU WA TANGANYIKA LEO, TUZIDISHE JUHUDI KATIKA KUFANYA KAZI ILI TUJILETEE MAENDELEO.

Tarehe 09/12/1961 Tanganyika ilikabidhiwa madaraka kamili ya kuiongoza nchi yao toka kwa wakoloni wa Kiingereza, Mwalimu J K Nyerere akateuliwa kuwa Waziri Mkuu wa kwanza wa Tanganyika huru, baadaye 1962 akawa Rais wa kwanza wa Jamuhuri ya Tanganyika kabla ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar 26/04/1964.

Tulinde amani na kuuenzi umoja wetu tunaojivunia kwa miaka mingi, tukumbuke historia wapi tumetoka na wapi tunaelekea, Mungu Ibariki Tanzania na watu wake. Amina.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni