Jumanne, 29 Mei 2012

MLIPUKO WA NAIROBI WAHUSISHWA NA UGAIDI WA KUNDI LA AL SHABAAB.



Mlipuko wajeruhi 33 Nairobi Kenya, polisi wasema huenda ni ugaidi
Polisi nchini Kenya inasema mlipuko uliojeruhi watu 33 katika mji mkuu Nairobi unaweza kuwa umesababishwa na bomu, baada ya hapo awali kulaumu hitilafu za umeme.
Mlipuko huo uliharibu maduka katika barabara yaMoi Avenuewakati wa mchana.Mtu mmoja aliyeshuhudia alisema kifurushi kiliachwa karibu yake kabla ya mlipuko kutokea.
Waziri Mkuu Raila Odinga amesema mlipuko huo unahusiana na magaidi.
Mwandishi wa BBC Kevin Mwachiro anasema mlipuko huo umesababisha bidhaa mbali mbali kama viatu, nguo na vioo vilivyovunjika kusambaa sehemu yote ya eneohilo.
Picha za Televisheni nchini humo zilionyesha watu wakikimbia mbali na majengo yaliyo karibu katikati ya mji waNairobi.
Awali Kamishna wa Polisi nchini Kenya Mathew Iteere, alisema huenda "hitilafu ya umeme" ndio chanzo cha mlipuko huo, kwa mujibu wa Televisheni ya NTV. Hata hivyo mlipuko huo unaiwekaNairobikatika hali ya wasiwasi.
Kumekuwa na milipuko kadhaa hivi karibuni ndani na nje ya mji huo mkuu huku baadhi ikihusishwa na kundi la wapiganaji wa Al-Shabaab.
Polisi waliweka kizuizi eneo la mlipuko huo Nairobi.
Timu ya waokoaji wa Shirika la Msalaba Mwekundu imetumwa katika eneo la tukio kwenye barabara ya Moi. Mtaa huo ni barabara kuu ambayo wakati wa mchana huwa na watu wengi, Shirika la habari la AP linasema.
Kwa mujibu wa watu walioshuhudia kulikuwa na mlipuko mkubwa na huku vipande vipande vya vioo na vitu vingine vikiwarukia na kujeruhi watu waliokuwa karibu, Gazeti la Nation linaripoti

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni