Jumanne, 3 Januari 2012

WAATHIRIKA WA MAFURIKO KUONDOLEWA KWENYE KAMBI ZA MASHULENI.

Mbunge wa Mafia Mh. Shaha akisaidia kuokoa waathirika wa mafuriko kwa Boti ya kukodi.


Hayo yamekuja ili kutakiwa kuwapisha wanafunzi wanaotarajiwa kufungua shule wiki ijayo nchini kote

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Saidi Meck Sadiki, alimesema Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Mgulani na Mbweni, limetoa nafasi za kuhifadhi waathirika hao baada ya kuondolewa katika kambi za shuleni
Amesema Shirika la Msalaba Mwekundu limeahidi kutoa mahema ya kutosha kwa ajili ya kuhifadhi waathirika hao Mabwe Pande na wanatarajia kuyafunga katika eneo hilo ndani ya wiki hii.

Amesema mahema hayo yatawahusu wenye nyumba waliopoteza nyumba zao na zoezi hilo halitawahusu wapangaji na hao kutakiwa kutafuta maeneo na kuondoka katika kambi hizo

Shule zinatarajiwa kufunguliwa Januari 9 mwaka huu, ambapo zilifungwa katika likizo ndefu iliyoanza mwanzoni mwa mwezi Desemba

NIFAHAMISHE ilitembelea kambi hizo na kupata maoni ya waathirika hao ambao walikuwa wamepanga na kutakiwa kuondoka katika kambi hizo na kusema kuwa, serikali haiwatendei haki kwani wao pia ni waathirika na kuiomba serikali iwafikirie japo wka nkwuapa msaada kidogo

Wamesema kuondoka katika kambi hizo kwa sasa itakuwa ngumu kwani hawana pa kuanzia na kuiomba serikali iwasaidie japo msaaada wa kuwapa kodi za pango japo ya mwaka mmoja ilki waweze kupanga.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni