Jumatatu, 16 Januari 2012

REGIA MTEMA KUAGWA KESHO KARIMJEE

Mbunge huyo alifariki juzi saa 5:15 baada ya kupata ajali mbaya ya gari katika eneo la Ruvu JKT, mkoani Pwani baada ya gari alilokua akiendesha kupinduka zaidi ya mara mbili.
Gari lililopata ajali na kusababisha kifo cha Mh. Mtema
Taarifa zilizotolewa na jeshi la polisi mkoani humo zilisema , marehemu Mtema alikuwa akiendesha gari aina ya LandCruiser namba T 296 BSM alipokuwa akitokea Dar es Salaam kuelekea mkoani Pwani.
Taarifa hiyo ilisema akiwa akiendesha gari hilo alipofika eneo hilo alitaka kulipita gari lililokuwa mbele yake lakini alishindwa kufanya hivyo ndipo gari lake lilipopinduka na kusababisha kifo chake.




Mh, Regia Mtema enzi za uhai wake.
Alisema Mtema alikuwa akiendesha gari aina ya Landcruiser lenye namba T 296 BSM, akitokea Dar es Salaam kuelekea Chalinze.
Taarifa zaidi zilieleza kwamba Mtema alikuwa anakwenda kukagua kiwanja chake mkoani humo na umauti kumfika njiani, pia marehehmu ameacha pacha wake ambaye alinusuruka na kifo hicho muda mchache tu alipomshusha pacha wake.
Mwili huo unatarajiwa kuagwa kesho katika viwanja vya Karimjee na kuzikwa keshokutwa huko Ifakara nyumbani kwao

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni