Jumapili, 8 Januari 2012

MTUHUMIWA WA MAUAJI AKAMATWA BAADA YA MIAKA MINNE.

JESHI la Polisi wilayani Nkasi limefanikiwa kumkamata mtuhumiwa wa mauaji, Charles
Mwananjela (38) maarufu kama `Topaz’.

Mtuhumiwa huyo alikuwa akitafutwa kwa takribani miaka minne.

Kamanda Isuto Mantage katikati.

Mtuhumiwa huyo anayedaiwa alikuwa dereva teksi na mkazi wa kitongoji cha Kipundu mjini Namanyere, Nkasi alikuwa anatafutwa na polisi tangu mwaka 2009 kwa tuhuma za mauaji ya
Mboje Masesa (60) mkazi wa Shishiyu, Shinyanga.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa , Isuto Mantage mtuhumiwa huyo alikamatwa juzi saa tisa mchana mjini Namanyere baada ya kuamua kurejea mjini hapo huku akidhani kuwa polisi walishasahau tukio hilo la mauaji.

“Mtuhumiwa huyu ambaye miaka minne iliyopita alikuwa dereva teksi mjini Namanyere anadaiwa kuwa alishiriki mauaji hayo yaliyotendeka Septemba 21, 2009 saa saba usiku katika pori lililopo katikati ya vijiji vya Mkole na Ipanda wilayani Nkasi.

“Yeye (mtuhumiwa ) akiwa pamoja na wenzake watano ambao tayari tumeshawakamata na kuwafikisha mahakamani walimshambulia mzee huyo pamoja na mkewe kwa marungu na kumuua pale pale,“ alisema Mantage.

Inadaiwa kuwa usiku huo wa tukio mtuhumiwa na wenzake hao pia walimshambulia mke wa marehemu ambaye alizirai kwa zaidi ya saa tano ambapo baadaye alizinduka akiwa hospitalini.

Kamanda Mantage alibainisha kuwa uchunguzi wa awali ulibaini kuwa mtuhumiwa na wenzake walikuwa wamekodiwa na Moshi Malambo ambaye alikuwa ni mfanyakazi wa marehemu,
akidaiwa kutaka kumrithi mke wa marehemu pia mali zake ikiwa ni pamoja na ng’ombe

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni