Ijumaa, 27 Januari 2012

BAADA YA KUHUSISHWA NA MASHTAKA NA ICC, UHURU KENYATTA AJIUZULU UWAZIRI.

Kenyatta aachia ngazi

Uhuru
Uhuru anakabiliwa na mashtaka kutoka ICC
Waziri wa fedha wa Kenya, Uhuru Kenyatta ameachia nafasi yake kufuatia uamuzi kuwa atashtakiwa kwa uhalifu dhidi ya ubinaadam.
Hatua hiyo inakuja baada ya Mahakama ya Kimataifa (ICC) kusema ajibu mashtaka kuhusiana na ghasia za baada ya uchaguzi nchini Kenya mwaka 2008.
Lakini atasalia kuwa naibu waziri mkuu, kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Rais Mwai Kibaki.
Afisa mwingine wa ngazi ya juu serikalini, Francis Muthaura, pia amejiondoa madarakani.
Wawili hao ni miongoni mwa watu wanne waliotajwa na ICC, ambao wote wanakanusha kuhusika kwao katika ghasia za uchaguzi mwaka 2007-08.
Mwanasheria mkuu wa Kenya alisema sio lazima kwa viongozi hao kujiuzulu, akisema hatma yao ingejulikana baada ya matokeo ya rufaa yao kupatikana ya kuzuia kesi ya Mahakama ya Kimataifa kuendelea.
Bw Kenyatta, ambaye ni mtoto wa rais wa kwanza wa Kenya Jomo Kenyatta, na ambaye anatajwa kuwa mmoja wa wananchi tajiri zaidi nchini humo, anatuhumiwa kwa uhalifu dhidi ya ubinaadam, ikiwemo mauaji na utesaji. Bw Muthaura anakabiliwa na mashtaka kama hayo pia.
Wawili hao ni washirika wa Rais Mwai Kibaki, ambaye alitoa wito kwa wananchi kuwa watulivu baada ya ICC kuthibitisha mashtaka yake dhidi ya watu hao.
Wanaharakati wamekuwa wakifanya kampeni kwa viongozi hao kuondolewa madarakani.
Mwandishi wa BBC mjini Nairobi amesema haijafahamika bado iwapo Bw Kenyatta ataachana na nia yake ya kuwania urais.
Zaidi ya watu 1,200 waliuawa katika wiki kadhaa za machafuko kati ya Disemba 2007 hadi Februari 2008, huku watu 600,000 wakilazimika kukimbia makazi yao. Wengi bado hawajapata makazi maalum hadi sasa.
Ghasia zilianza baada ya kuzuka mapigano kati ya wafuasi wa wagombea urais Raila Odinga na Mwai Kibaki, na baadaye kufikia kuuana katika misingi ya kikabila.
Waziri wa zamani wa elimu William Ruto na mtangazaji wa redio Joshua arap Sang, ambao walimpinga Bw Kibaki mwaka 2007, pia wanashtakiwa katika kesi nyingine

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni