Jumapili, 22 Januari 2012

DUKA LA VINYWAJI BARIDI LANUSURIKA KUUNGUA MOTO STENDI YA MABASI NACHINGWEA JANA USIKU.


Viti vya plastiki vilivyoungua ndio bidhaa pekee iliyoathirika na moto huo.

Kumekuwa na tabia au dhana ya kulitaja sana Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kuwa linahusika sana na kusababisha moto sehemu mbalimbali, lakini jana Mambobado ilishuhudia moto katika moja ya vibanda vya biashara kuzunguka Stendi kuu ya mabasi Nachingwea mida ya saa tano usiku uliosababishwa na mkaa wa moto uliohifadhiwa ndani ya kibanda hicho kwa ajili ya matumizi ya siku inayofuata.

Wasamaria wema wakishuhudia tukio hilo mara baada ya kuzimwa kwa moto huo ambao ulisababisha hasara kidogo maana ulizimwa kabla haujakolea na pengine kuhamia vibanda vingine. Ilibidi wasamaria wema wavunje mlango huo baada ya kusikia harufu ya vitu vinavyoungua na mwanga wa moto kuonekana kwa ndani, mwenye mali alijulishwa baadae na alikuta vitu vyake salama.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni