Jumamosi, 21 Januari 2012

TAMKO LA VIONGOZI WA JUMUIYA YA WANAFUNZI NA VIJANA WA KIISLAMU TANZANIA

IN THE NAME OF ALLAH, THE ALL-COMPASSIONATE, ALL - MERCIFUL
TANZANIA MUSLIM STUDENTS AND YOUTH ASSOCIATION (TAMSYA)
HEAD OFFICE
P.O BOX 35491,
DAR ES SALAAM
TANZANIA –EAST AFRICA 
Website: www.tamsya.org Email: info@tamsya.org
Phone: +255732994703 Fax: +255732994703 Mobile: +255715 944514
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

NDUGU WANAHABARI
Awali ya yote hatuna budi kumshukuru Mwenyezi Mungu mola wa viumbe wote. Pili tuna kushukuruni kwa kuitikia wito wetu licha ya kuwa na majukumu mengi ya kutoa taarifa kwa wananchi.Kwa mara ya kwanza tumeamua kukutana nanyi. Nasi tunatoa taarifa yetu hii kwenu ili muifikishe kwa Watanzania na wapenda amani wote duniani. Tunakuusieni
juu ya ukweli na uaminifu katika kuripoti taarifa hii.Tuna kuusieni tena kuripoti taarifa hii bila ya kupotosha maana iliyokusudiwa.Kutakuwa na nafasi ya maswali ili kuuliza ikiwa kunasehemu ambayo haikueleweka.

NDUGU WANAHABARI
Tuliowaita ni viongozi wa Jumuiya ya Wanafunzi na Vijana wa Kiislamu Tanzania yaani Tanzania Muslim Students & Youth Association (TAMSYA).Jumuiya yetu inatambulika kisheria na inafanya kazi zake kwa kufuata sheria za nchi.

NDUGU WANAHABARI
Jumuiya yetu kama inavyojieleza inashughulika na malezi ya wanafunzi wafuasi wa dini ya kiislamu waliopo katika shule, vyuo vya kati na vyuo vikuu na vijana wa kiislamu kwa ujumla. Jumuiya hii inawalingania waishi kwa mujibu wa mafundisho ya dini ya Uislamu.

NDUGU WANAHABARI
Tumeamua kukutana nanyi ili kuzungumzia mambo ambayo yanawapata wanafunzi waislamu waliopo kwenye shule na vyuo vya serikali kwa muda mrefu. Wanafunzi waislamu wamekuwa wakinyanyaswa na kuwekewa vipingamizi vya makusudi ambavyo vinasababisha kufanya vibaya katika masomo yao pindi wakiwapo shuleni.

NDUGU WANAHABARI
Sheria ya nchi inaruhusu uhuru wa kuabudu na kuchagua dini. Kwa mujibu wa dini yetu ya uislamu ibada haimaliziki kwa kuingia msikitini nakuswali tu bali Uislamu wenyewe ni mfumo kamili wa maisha. Ibada ni kila jambo analolifanya muislamu na linaloridhiwa na Mwenyezi Mungu likiwa katika muundo wa vitendo au kauli za dhahiri na kificho.

NDUGU WANAHABARI
Tumepata malalamiko kutoka kwa wanafunzi waislamu wakikatazwa kuvaa
HIJABU shuleni,,Tumepata mashitaka kutoka kwa wanafunzi waislamu wakinyimwa sehemu za kusalia/kufanya ibada ya sala katika mazingira ya shule na vyuo. Tumepata mashitaka juu ya kupangwa makusudi matukio mbali mbali ya shule katika nyakati za sala za waislamu. Mfano sherehe za Mahafali zinapangwa kufanyika siku za Ijumaa muda wa sala, Ratiba za mitihanivyuo vikuu hazizingatii muda wa swala ya Ijumaa .kurefusha muda wa
kusimama mstarini (Parade) mpaka muda wa swala unapita.

Wanafunzi waislamu wamekuwa wakikatazwa kuvaa kofia au kanzu baada ya muda wa masomo katika shule za bweni huku wakristo wakiwa wanashinda
na Rozari masaa 24. Waalimu wanaofundisha somo la maarifa ya uislamu wanawekewa vikwazo mbalimbali wakati wachungaji wanapishana katika shule bila vikwazo
kwenda kufundisha baibal knowledge.

Vipindi vya dini vinawekwa katika ratiba za shule muda wa saa saba
mchana siku ya ijumaa wakati ambao wanafunzi wa kiislam wanapaswa
kuenda msikitini kwa ajili ya swala ijumaa.

NDUGU WANAHABARI
Tutatoa mifano kadhaa katika maeneo tofauti ambayo wanafunzi waislam
wamefanyiwa madhila, manyanyaso na udhalilishwaji ikiwa ni pamoja na
kutukaniwa Mungu wao,mtume wao na kitabu chao (Quran tukufu) na TAMSYA
imefuatilia bila ya mafanikio.

SHULE YA SEKONDARI KIZUNGUZI WILAYANI KILOSA –MOROGORO
Mwanafunzi wa kidato cha nne, Frank Thobias Cosmas, aliandika waraka ulioukashifu uislamu, Qurani tukufu na Mtume Muhammad Sallalahu alaihi wasallam.Wakati wanafunzi wakristo wakiwa wanaubandika katika mbao za matangazo shuleni hapo na kusambaziana waraka huo Tarehe 13/05/2011 mwanafunzi muislamu Saidi Suleiman aliupata na kuufikisha kwa viongozi wa wanafunzi waislamu na hatimaye malalamiko hayo yalifika kwa mkuu wa
shule.

Mkuu wa shule alimpa Adhabu Yule mwanafunzi aliye peleka taarifa na viongozi wa wanafunzi waislamu walisimamaishwa shule kwa muda wa siku 21, na Yule aliyendika waraka huo alibakishwa kufanya kazi za shule.Tukio hili liliripotiwa kwa Mkuu wa polisi Morogoro, Afisa Elimu Mkoa Morogoro na ofisi ya mkuu wa wilaya ambao walipuuza. Hatua hiyo
ilisababisha waislamu wa Mkoa wa Morogoro kuandamana kwa amani siku ya
Ijumaa tarehe 5 Agosti, 2011.

PIA SHULE YA SEKONDARI ULONGONI – DAR ES SALAAM Siku ya Alhamisi,tarehe 27/01/2011Mkuu wa shule hiyo aliwalazimisha wanafunzi wa kike wa shule hiyo kuvua Hijabu wakati wa zoezi la kupigapicha kwa ajili ya Mtihani wa kidato cha nne.Alifanya hivyo kwa chuki za udini kwa sababu waraka wa baraza la mitihani unaotoa maelekezo ya
namna na utaratibu wa kupiga picha kila mkuu wa shule amepatiwa na
haukuagiza hivyo.


SHULE YA SEKONDARI ENGUSERO KIBAYA –KITETO
Mkuu wa shule hiyo kwa kushirikiana na Kaimu katibu Mkuu wa mkoa wa Manyara kwa barua yake ya Kumb.Na.FA.58/347/01/27 aliwaamrisha wanafunzi wavunje msikiti uliopo hapo shuleni kwa madai ya kwamba katika shule za serikali hairuhusiwi kujengwa nyumba ya ibaada. 

Lakini
sikweli kwa kuwa zipo shule nyingi za serikali zilizo na nyumba za ibada makanisa tena makubwa sana. Mfano Shule ya sekondari Ndanda, Shule ya sekondari Umbwe, Lyamungo Sekondari, Pugu Sekondari Dar es salam na karibu shule zote kubwa za Serikali nchini. Huu ndio udini na mfumo kristo unaolalamikiwa na unaoliyumbisha taifa.

SHULE YA SEKONDARI ALDERSGATE BABATI MANYARA Mkuu wa shule hiyo aliwanyima wanafunzi waislamu darasa kwa ajili ya kusomea somo la maarifa ya uislamu na kuwaambia kama wanataka kusoma somo la dini wachanganyike na wakristo ambao wamepewa chumba cha kusomea shuleni hapo, Jambo ambalo ni kinyume na sheria na kanuni za nchi.aidha alipiga marufuku uvaaji wa hijabu shuleni hapo kwa taarifa
tuliyo letewa ya 17/03/2011.

SHULE YA SEKONDARI LUGOBA
Mwalimu aliwataka wanafunzi waislamu washerehekee Krismas walipokataa akawaambia tutaweka Taarabu maana waislamu mnapenda sana taarabu.

Siku ya 21/01/2011 kwa makusudi Makamu Mkuu wa shule hiyo aliingia na viatu katika eneo la chumba wanachotumia waislamu kuswalia na kuwaamuru watoke katika chumba hicho wakati wa swala.

Makamu Mkuu huyo alikwenda tena siku ya tarehe 31/01/2011 kwa hasira na kundi kubwa lililo sheheni wanfunzi wakristo kwa ajili ya nkuwafanyia fujo waislamu waliokuwa wakiswali. jambo ambalo lileta tafrani kubwa shuleni hapo cha kusikitisha ni kuwa ukweli ulipotoshwa
na hatimaye wanafunzi waislamu walionekana ndio chanzo cha tatizo.

SHULE YA SEKONDARI ILBORU ARUSHA
Mwanafunzi Juma Hassan alifukuzwa shule 13/01/ 2006 ikiwa ni wiki tatu kabla ya kuanza kwa mitihani ya kidato cha sita. Sababu ya kufukuzwa shule ilidaiwa alimsukuma Mama Mkwizu mwalimu sheleni hapo alipotaka kuingia msikitini.

SHULE YA UFUNDI TANGA JIJINI TANGA
Mwaka 2006 Mkuu wa shule hiyo bwana T. Z. Kinala amekuwa na tabia ya Kutoa salamu ya HALELUYAH mstarini wakati wa PAREDI huku akijua kwamba wanafunzi walio mbele yake ni mchanganyiko wa waislamu,wakristo na watu wa dini nyingine.

Lakini si hivyo tu, Tarehe 24/7/2006 mkuu wa shule alileta kikundi cha
kwaya cha kanisa wakati PAREDI na kuimba nyimbo za ibada ya kikristo.

Wakati alipo kuwa akiongea na wanafunzi wa, katika hafla fupi ya kuwakaribisha kidato cha tano mnamo tarehe 28/4/2006 Pia alitamka wazi wazi kuwaambia wanafunzi waislamu kuwa hapa shuleni hakuna kuswali swala tano kwani hii siyo seminari.

Mnamo tarehe 18/06/2006 aliwaambia wanafunzi wa kiislamu wanaovaa mavazi yanayotambulisha uislamu wao, kama Kofia, Kanzu na Kilemba lau kama angeliwajua asingewachagua kujiunga na shule yake.

Mnamo tarehe 02/08/2006 aliwaita waislamu wanaovaa mavazi ya kiislamu
kama kanzu kuwa ni Mashoga

NDUGU WANAHABARI CHUO KIKUU CHA DODOMA (UDOM)
Madhila haya na manyanyaso hayawasibu wanafunzi wa kiislam waliopo mashule tu lakini hata wale waliopo vyuo na vyuo vikuu pia hawajasalimika hapa tutatoa mfano wa chuo kimoja tu cha Dodoma (UDOM) ambako wanafunzi wa kiislam chuoni hapo wamekuwa wakidhalilishwa, kwa kutukaniwa dini yao na mtume wao mfano wa haya ni mwaka jana wakati wa kampeni za uchaguzi wa serikali ya wanafunzi ambapo yalibandikwa matangazo yenye ujumbe unaowatukana na kukejeri uislam na waislam kuwa ni watu wasioweza na wasiostahiki kuongoza,jambo ambalo liliwafanya wanafunzi wakiislam chuoni hapo kuripoti katika uongozi wa chuo na vyombo vya usalama bila ya kupewa msada, hatimae waislam waliamua kujitowa katika mchakato huo wa kampeni na uchaguzi wakiwa na nia
njema ya kujiepusha na uadui na uhasma baina yao na wanafunzi wa dini zingine, lakini hata hivyo baada ya uchaguzi walitukanwa na kukashifiwa wazi wazi na wakirsto wakishangilia kwa kusema Yesu ameshinda na Mohammad ameshindwa katika kona zote za chuo, bila ya
kuchukuliwa hatua za kisheria na mamlaka husika za chuo na serikali.

NDUGU WANAHABARI
Tukio kubwa na la kusikitisha kwa wakati huu ni hili la shule ya sekondari NDANDA iliyopo mkoa wa MTWARA wilaya ya Masasi tarafa ya Chikundi kata Mwena kijiji cha Ndanda. Mpaka hivi sasa tunapozungumza nanyi wanafunzi ishirini (20) wa kiislamu wamefukuzwa shule watano (5) wakiwa ni kidato cha tano na kumi na tano ni kidato cha sita ambao
wanatarajiwa kufanya mtihani wa mwisho mwanzoni mwa mwezi wa pili.

Aidha wengine waliosalimika kufukuzwa shule wamewekewa masharti magumu
ya kusaini ikiwa wanataka kuendelea na shule hiyo ya serikali.Miongoni
mwa masharti hayo ni kutojihusisha na dini yao wakiwa shuleni sharti
ambalo linapora haki ya kikatiba ya kuabudu.
Sababu na kosa la kufukuzwa wanafunzi hao wa kiislam likiwa ni kuuomba
uongozi wa shule uwape eneo maalumu la kufanyia ibada (Msikiti) kama
vile walivyotengenezewa wanafunzi wakirsto kanisa kubwa shuleni hapo,
kulalamika lugha za kashfa na dharau ambazo zinatolewa na mkuu wa
shule dhidi ya wanafunzi wa kiislamu uislamu shuleni hapo.

Kilichowaponza wanafunzi waislamu ni kupinga udini wa mkuu wa shule na
upendeleo kwa wanafunzi wakristo, mfano kitendo cha mkuu wa shule
kuteua viongozi wa serikali ya wanafunzi kiholela na kiupendeleo kwa
wakirsto huku wakitoka nje ya shule wakishangilia na kusema Muhammad
ameshindwa katika uchaguzi mwache bwana Yesu atawale shule!!! Haya
yamefanyika mkuu wa shule akiyaona bila ya hata kukemea na
kuwaadabisha wanafunzi wahusika jambo ambalo linaonesha wazi wazi kuwa
ni mpango maalum ulio sanifiwa kwa mfumo maalum.

NDUGU WANAHABARI
TAMSYA mikoa, wilaya na matawi, shule na vyuo kwa muda mrefu imefanya
jitihada mbalimbali za kuonana na wakuu wa shule na watendaji husika katika kadhia hizi na kuishia kupuuzwa bali na kupewa majibu ya kejeli na jeuri. Na baadhi ya wakuu wa shule kuomba msamaha na kuahidi kutorudia tena, lakini baada ya muda mfupi hurejea na kuendeleza dhulma na madhila kwa wanafunzi wakiislam kwa kasi ya ajabu.

Pia walimu walezi wa wanafunzi wa kiislamu au hata walimu waislamu wanao thubutu kuhoji juu ya ubaguzi wa kidini pia huonekana vioja huku wakichekwa na hatimae kupewa adhabu ya kuhamishwa kituo cha kazi kiholela mfano dhahiri ni walimu wawili pekee wakiislam wa Ndanda Sekondari ambao wamefungashiwa virago vyao na kupelekwa vijiji vya
mbali kosa lao likiwa ni kutaka haki itendeke baina ya wanafunzi wote, na wakati mwingine walimu waislam hujikuta wakiambulia vichapo na vipigo kama alivyofanyiwa mwalim Halima wa Ifunda sekondari palen alipopinga dhulma, uonevu na udhalilishwaji dhidi ya wanafunzi waislamshuleni hapo mwaka 2009 akajikuta anaambulia kipigo kutoka kwa mwalim
wa kikristo.

NDUGU WANAHABARI
Hapa tumeonesha sehemu ndogo ya madhila yanayowasibu wanafunzi wa kiislam nchini kama mifano tu. kwani ni vigumu kueleza madhila ya kila shule au chuo kwa njia hii. Jambo la faraja ni kuwa kila mtanzania anajua haya hata watu wa kawaida pia
.
Kwa kuwa tatizo hili ni la muda mrefu na baadhi ya viongozi wa serikali mfano Rais mstaafu wa awamu ya Tatu Mh. Benjamin Mkapa alipoulizwa juu ya hali ya uwiano wa waislamu na wasiokuwa waislam katika sekta ya elimu alikiri kuwepo matatizo na uduni kwa upande wa
waislam na matatizo mengi huku akisema kuwa si kosa la serikali bali
ni tatizo la kihistoria.

Sisi wanafunzi wa kiislam Tanzania tunasema wazi na tunao ushahidin kuwa hili si tatizo la kihistoria bali ni mpango maalum uliosanifiwa na serikali ya awamu ya kwanza kwa lengo la kuwadhulumu na kuwakandamiza waislam kielimu kwa mbinu mbalimali kama hizi
zilizotumiwa na uongozi wa shule ya sekondari Ndanda na wanaharakati wengine wa mfumo kiristo katika sekta zote za elimu nchini.

Wanafunzi wa kiislamu Tanzania tunajua kuwa kitendo kilichokifanywa na mkuu wa shule ya Ndanda na Bodi ya shule pamoja na maafisa elimu cha kuwafukuza shule wanafunzi ishirini (20) wa kiislam na wengine
  
kuwekewa masharti magumu ya kuacha wito wa dini yao ili waruhusiwe
kurudi shuleni si kitendo kipya bali ni muendelezo wa dhulma ambayo
walifanyiwa babu na baba zetu ambapo walilazimishwa wachague aidha
kuacha dini au kusoma, Alhamdul llah tunashukuru kwa kiasi Fulani
walifanya maamuzi magumu ya kulazimika kuacha kusoma na kubaki na dini
yao kwani kama wangechagua la pili basi huenda nasi leo tusingekuwa
katika dini ya haki ya uislam.

Ama leo hii sisi wanafunzi wa kiislamu Tunasema kusoma ni sehemu ya dini yetu kama tulivyoamrishwa na Allah (sw) Quran (96:1-5) kwa hiyo hatutokubali tena kuacha wito wa dini yetu kwa kutenganisha dini na elimu kwani ikiwa tutafanya hivyo basi itakuwa tumefanya dhulma kubwa
kabisa.

Hapa tunawapongeza wanafunzi wa kiislam wa Ndanda sekondari kwa kujitambua na kujua haki zao za kiiman na kikatiba kwa kutoutii uongozi wa kidhulma wa shule ya ndanda pale ulipowalazimisha kuacha wito wa dini yao ili wasome, wanafunzi wa Ndanda wamefanya jambo tukufu linalopaswa kuungwa mkono na kuigwa na kila mtu mwema. Na napenda kutoa wito kwa wanafunzi wakiislam nchini kote ya kuwa wanapaswa kuwaiga na kuungana na ndugu zao zao wa Ndanda sekondari kwa kutokubali dhulma ya namna yoyote ile.

NDUGU WANAHABARI
Kadhia ya Ndanda ni mzito sana ambayo imegusa hisia ya kila muislam na kila mtanzania mpenda amani na haki, ukweli wa hili unathibitika wazi wazi kwa kila mwenye uhuru wa kufikiri kwani vijana wale wa kidato cha sita waliofukuzwa ni nguvu kazi muhimu sana kwa ujenzi wa taifa ambao tayari kusoma kwao wangeweza kuiokomboa jamii na taifa kiujumla.
Lakini jambo la kusikitisha ni kuona viongozi wenye dhamana katika wizara ya elimu wakilichukulia swala hili kisiasa kinyume na uhalisia wake. Kwa kufanya ziada na uchunguzi wa kubahatisha bila umakini hatimae kutoa taarifa zilizojaa usiasa ndani yake, kuwa eti maamuzi ya bodi ya kuwafukuza wanafunzi (20) wa kiislam ni sahihi huku akieleza
kuwa amefika Mtwara na kuongea na Bodi ya shule, mkuu wa shule, walimu na serikali ya wanafunzi hatimae wanafunzi wote Paredi bila ya kuwaruhusu kuuliza maswali au kutoa maoni yao hatimae kutoa hukumu.

Hukumu hii haiwezi kuwa sahihi kwani hajawashirikisha wahusika wa upande wa pili wa mgogoro ambao ni wanafunzi wa kiislam kwa kuwasikiliza hoja zao madai yao ya msingi, huku ni kuisaliti katiba ambayo wameapa kuilinda ambayo inarususu uhuru wa kutoa mawazo na kila mmoja kuheshimiwa kwa nafasi yake. Jambo zito zaidi ni kuona naibu waziri anaungana na watu madhalimu waliovunja katiba ya nchi kwa kuwalazimisha wanafunzi kuacha wito wa dini yao ili warudi shule sharti hili linavunja katiba Ibara ya (19:1-2) kinachozungumzia uhuru
wa imani na kuabudu.

Kutokana na uzito na unyeti wa kadhia hii na madhila haya yanayoendelea kufanywa dhidi ya wanafunzi wa kiislam nchini leo hii tunapenda tuutangazie uma kuwa sasa basi hatutaki kuendelea tena kudhulumiwa na kunyanyaswa, sisi ni watanzania na tuna haki zote kama
wanajamii wengine.

Kwahiyo tumeitaka serikali ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania kufanya
mambo yafuatayoTunaitaka wizara ya elimu kuwarejesha wanafunzi wote walofukuzwa na
wengine bila masharti yeyote ndani ya siku tano (5) kuanzia tarehe
13/01/2012.

Tunaitaka serikali kuunda Tume huru itakayo chunguza kero wanazopata
wanafunzi waislamu katika shule za serikali nchi nzima.

Tunaitaka serikali kuwawajibisha watendaji wa sekta ya elimu wanaoendekeza udini ubaguzi na unyanyasaji kwa wanafunzi wa kiislamu.

Tunaitaka serikali ithibitishe au ikanushe juu ya madai ya mkuu wa shule Ndanda na badhi ya viongozi wa serikali kuwa mashule yaliyotaifishwa na serikali, serikali inamiliki majengo tu ama ardhi na mamlaka ya matumizi yake yako chini ya Taasisi zake za asili.

Shule zote za serikali zitenge maeneo malum ya kufanyia ibada kwa ajili ya watu wa dini zote. Asilimia kubwa ya wakuu washule za sekondari za serikali ni wakristo, hivyo basi tunaomba serikali iweke mgawanyo sawa wa nafasi hizo.

Kila jambo linapaswa kuwa na mwisho, hatuwezi kuendelelea kuvumilia uonevu wa wazi wazi siku zote.Hatuwezi tena kuendelea kuishi kamawanafunzi daraja la pili katika nchi yetu.
Lazima haki sawa na uhuru upatikane kwa wanafunzi wa dini zote na sio kukandamiza waislamu. Hivyo basi tunalazimika kupaza sauti zetu kwa kuingia barabarani kuonesha hisia zetu katika hali ya unyonge wetu

NDUGU WANAHABARI
Tunakusudia kufanya maandamano ya amani nchi nzima 20 Januari 2012 ambayo yatapeleka ujumbe kwa kila kiongozi wa Elimu katika mkoa yaani Afisa Elimu Mkoa na waislam wa Mkoa wa Dar es salaam watapeleka ujumbe moja kwa moja kwa waziri wa elimu.Kwa lengo la kutaka azingatie madai yetu ya kutonyanyaswa na kubaguliwa katika shule ya serikali.Lakini hatutoishia katika maandamano iwapo hali ya ubaguzi haitokoma.Tutatumia njia nyingine za kujikomboa katika madhila haya.

Tunasema “tumenyanyaswa,tumedhaliliswa, tumebaguliwa kwa miaka 50 ya uhuru na tukavumilia na kusubiri vyakutosha leo tunasema inatosha na tumechoka tunaitaka serikali itambue haki,heshima na utu wetu kama wanavyoheshimiwa wanafunzi wa dini zingine mashuleni na mavyuoni.”

Tunataka tuheshimiwe kama wanaadamu, kama wanatanzania huru, wanafunzi halali mashuleni na vyuoni kama wananyoheshimiwa wanafunzi wa dini zingine. Tumeanza muda mrefu kudai haki zetu kwa njia za kidiplomasia lakini hatujasikilizwa na leo tunatumia njia nyingine ya kidiplomasia na kikatiba ambayo ni MAANDAMANO ya amani huenda kwa njia hii serikali na jamii itasikia kilio chetu.

 ACHENI KUTUDHALILISHA NA KUTUNYANYASA WANAFUNZI WA KIISLAM MASHULENI NA MAVYUONI SASA BASI INATOSHA TUNAOMBA WAISLAM WOTE NA WAPENDA AMANIWOTE MTUUNGE MKONO KATIKA MAANDAMANO HAYA YA AMANI.

Ahsanteni. 

JAFARI SAIDI MNEKE 
RAISI WA JUMUIYA YA WANAFUNZI NA VIJANA
WA KIISLAMU TANZANIA (TAMSYA)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni