Jumatatu, 5 Agosti 2013

RAIS ZUMA WA AFRIKA YA KUSINI AMPONGEZA RAIS ROBERT MUGABE KWA KUSHINDA UCHAGUZI 2013.


Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini ametoa zile alizoita, hongera nyingi kwa Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe, ambaye ameshinda muhula wa saba wa uongozi akiwa na umri wa miaka 89.
Zuma akikaribishwa na Mugabe alipozuru Harare zamani

Rais Zuma amesema uchaguzi mkuu wa Zimbabwe ulifanikiwa, na ametoa wito kwa pande zote zikubali matokeo.
Mpinzani mkuu wa Bwana Mugabe, Morgan Tsvangirai, mwenye umri wa miaka 61, amekataa matokeo na amesema atapeleka malalamiko mahakamani.
Viongozi wa mataifa ya magharibi yamesema yana wasi-wasi kama uchaguzi ulikuwa wa halali.
Bwana Mugabe alipata asili-mia-61 ya kura katika uchaguzi wa rais.
Na chama chake cha ZANU-PF kilipata thuluthi mbili ya viti vya bunge

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni