Jumamosi, 7 Aprili 2012

R.I.P STEVEN KANUMBA

STEVEN KANUMBA AFARIKI DUNIA





Nimeshtushwa na message nilizozipata katika simu yangu toka kwa dada Rehema Fredrick Fussi(Mama Latif) alfajiri ya leo kuelezea kifo cha Steven Kanumba na ndipo nilipokurupuka usingizini na kuanza kuwapigia ndugu na jamaa zangu wa karibu lakini wakati nikifanya yote hayo ndipo nilipoingia katika mtandao wa jamii (facebook) na kukuta salamu za msiba, nilishikwa na mshangao na bumbuwazi, taarifa zilianza kuenea jijini Dar es salaam kiasi cha saa nane na nusu usiku kuwa Steven Kanumba amefariki. Habari ambazo zina uhakika ni kuwa maiti yake ilikuwa tayari imekwishapelekwa mochwari Muhimbili. Sababu ya kifo bado ni utata kwani kuna maelezo kuwa alianguka ghafla, kukiwa na maelezo mengine kuwa alifariki usingizini. Na wengine wanasema amepata ajali. Pamoja na yote Mungu Amlaze Pema Kanumba, tulimpenda lakini Mungu amempenda zaidi

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni