Jumapili, 8 Aprili 2012

MH. CHIKAWE(MB) ATEMBELEA HOSPITALI YA WILAYA NACHINGWEA KUKAGUA JENGO LA MAABARA, KUONA WAGONJWA NA KUTOA MSAADA WA VIFAA JUMAMOSI YA PASAKA.

Mh. Chikawe akiwasili eneo la hospitali na kusalimiana na wadau mbalimbali wa afya wilayani Nachingwea hapo jana asubuhi.
Mh. Chikawe akisalimiana na mgonjwa mmojawapo katika wadi ya wanaume ambaye amevunjika mguu na mkono baada ya kupigwa na majambazi hivi karibuni. Pia Mh. Chikawe aliahidi kumsaidia usafiri na masurufu mzazi wa mtoto Khatibu Hashim(4) anayesumbuliwa na uvimbe kichwani na kapata rufaa kwenda Muhimbili Hospitali ya Dar es Salaam.
Hapa ni ndani ya jengo jipya la maabara, limejengwa kwa msaada toka Clinton Foundation ya Marekani.
Hapa akikabidhi vifaa mbalimbali ikiwemo kitanda cha kuzalishia na baiskeli ya kukalia wagonjwa.
Hapa Daktari Mfawidhi wa Nachingwea akipeana mkono na Mh. Chikawe kama ishara ya kumshukuru kwa msaada wake huo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni