Jumapili, 29 Aprili 2012

KADA WA CHADEMA ACHINJWA HUKO ARUMERU.


MWENYEKITI wa Chadema wa kata ya Usa River w i l a y a n i Arumeru mkoani hapa, Msafiri Mbwambo (32) mkazi wa Lake Tatu, ameuawa kwa kuchinjwa na kiwiliwili kutelekezwa makaburini na watu wasiojulikana.

Tukio hilo linalohusishwa na masuala ya kisiasa, lilitokea juzi saa tatu usiku eneo la Mukidoma,
Usa River, ambako wauaji wanadaiwa kutumia panga kumchinja Mbwambo na kutokomea.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, walidai kuwa kabla ya tukio Mbwambo alikuwa na wenzake wakistarehe kwa vinywaji, lakini yeye hakuwa anakunywa chochote lakini ghafla alipigiwa simu na watu hao, wakidai kuwapo wanachama wa CCM waliotaka kurudisha kadi na kujiunga na Chadema.

Taarifa zilidai kuwa Mbwambo alichukua pikipiki na kuwafuata, lakini hakurudi hadi mwili wake ulipokutwa umetelekezwa kando ya barabara makaburini, pikipiki na vitu vingine vikiwa eneo hilo bila kuchukuliwa na wauaji.
R I P Mbwambo.
Hata hivyo, chanzo cha tukio hilo hakijajulikana ila taarifa za awali zinahusisha masuala ya
kisiasa, kwani baada ya uchaguzi mdogo wa ubunge Arumeru Mashariki kumalizika, malumbano ya kisiasa na kukamiana yaliendelea eneo hilo.

Katika uchaguzi huo wa Aprili mosi, Joshua Nassari wa Chadema aliibuka mshindi akimbwaga
mshindani wake mkubwa, Sioi Sumari wa CCM baada ya jimbo hilo kumpoteza mbunge wake,
Jeremiah Sumari ambaye ni baba mzazi wa Sioi.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha, Thobias Andengenye, alithibitisha kutokea tukio hilo
na kudai kuwa, polisi bado wanafanya uchunguzi na hadi sasa hakuna mtu anayeshikiliwa na mwili wa marehemu umehifadhiwa katika mochari ya hospitali ya mkoa ya Mount Meru kwa
uchunguzi zaidi

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni