Jumanne, 28 Februari 2012

PADRI WA KANISA AWASIMANGA WAKWERE WA LUGOBA.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete wa Tanzania, Naye ni Mkwele wa Lugoba Bagamoyo.
Padri Mkude alizuiwa kuongoza misa jana asubuhi parokiani hapo, baada ya waumini zaidi ya 200 kuandamana wakiwa na mabango zaidi ya 20 wakidai ahamishwe kwa kuwa amewatukana katika mahubiri yake, kwamba watoto wao ni wachafu na wao wamebaki kucheza ngoma badala ya kufanya maendeleo.

“Tumechoka na mahubiri ya huyu Padri, kila akihubiri kanisani lazima atuseme Wakwere,
tumemkosea nini? Mara atuseme tu masikini, mara watoto wetu wachafu na hatuwapeleki shule tunashindia ngoma, tumechoka, hatumtaki,” alisema muumini ambaye hakupenda jina lake liandikwe gazetini.

“Leo tumemzuia asisome misa kabisa, hakuna haja maana hakuna amani kanisani, hatujui ana kitu gani na sisi, sijui kwa sababu parokia hii ipo kwa Wakwere? “Hata Jumatano ya Majivu wiki iliyopita katusema tena, eti watoto wetu ni wachafu sana ukilinganisha na makabila mengine, hii ni kashfa.”

Wakwere ni moja ya makabila katika Mkoa wa Pwani linalopatikana wilayani Bagamoyo, Pia Rais wa Tanzania ni Mkwere. Muumini mmoja alidai mahubiri ya Padri huyo ya kuwasema Wakwere hayakuanza siku za karibuni, bali ni ya muda mrefu na yamekuwa kama ya kusutwa badala ya kulishwa Neno la Mungu.

“Hali hiyo imesababisha watu kutokwenda kanisani wakijua leo Padri huyo anaongoza misa, lakini akiongoza Katekista, misa inajaa utadhani Askofu amekuja, tunachotaka hapa ni Padri mwingine, kama Askofu anatujali atuletee mwingine,” alisema muumini huyo

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni